• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo azihimiza Halmashauri kuongeza mashine za mapato kuongeza ukusanyaji

imewekwa Tar: November 17th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amezihimiza Halmashauri zote Mkoani humo kuhakikisha zinaongeza idadi ya mashine za EFD ili kuongeza ukusanyaji wa mapato yao katika halmashauri.

Amesema kuwa kwa mwaka wa fedha 2016/2017 Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ilikisia kukusanya Shilingi bilioni 2.3 ambapo hadi sasa Wilaya imekusanya Shilingi bilioni 1.9 ikiwa ni ongezeko la asilimia 97 katika makusanyo ya ndani ya Halmashauri hiyo.

“Halmashauri Ziongeze hizo mashine, kama mnavyofahamu serikali hii inahimiza ukusanyaji wa mapato ya ndani kwa kutumia mfumo wa Kielektroniki, wenyewe mmekuwa mashuhuda mmevuka kile kiwango mlichojiwekea na kupata ongezeko la asilimi 97 kama mlivyosoma kwenye taarifa yenu, mkiongeza mashine hizo zikafikia idadi inayotakiwa makusanyo ya ndani yatakuwa mengi zaidi,” Alieleza.

Ameongeza kuwa makusanyo ya ndani yakiwa mengi zaidi itasababisha shughuli za kimaendeleo kufanyika kwa wingi zaidi, ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa, huku upungufu wa vyumba hivyo ukiwa ni 1399.

Ameyasema hayo baada ya kusomewa taarifa ya Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga katika Ziara yake ya siku mbili yenye lengo la kutembelea miradi mbalimbali, kujitambulisha kwa watumishi pamoja na kuongea na makundi mbalimbali ya wananchi katika halmashauri hiyo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa H/W ya Sumbawanga John Msemakweli amesema kuwa hadi sasa Halmashauri ina mashine za Kielektroniki 64 na uhitaji ni mashine 114 na kusababisha upungufu wa mashine 50 huku akiahidi kuzikamilisha ili kuweza kuongeza mapato ya Halmashauri hiyo.

“Tuna upungufu wa vyumba vya madarasa 1399 na hadi sasa kwa mpango wa kujenga vyumba vitatu kwa kila shule tuna vyumba 98 ambavyo vipo usawa wa linta na kwengine tunaendelea kuwahamasisha wananchi kuweza kuchangia katika ujenzi,” Alisema.

Nae Mh. Wangabo aliwaagiuza kuangalia upya mpango wao wa ujenzi wa madarasa hayo kwani itawachukua muda mrefu ikiwa watajenga madarasa 98 kwa mwaka.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • KIWANJA CHA NDEGE SUMBAWANGA KUKAMILIKA MACHI 2025

    October 02, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa