• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

REA KUANZA KUSAJILI NA KUUZA MAJIKO BANIFU MKOANI RUKWA

imewekwa Tar: August 28th, 2025


Sumbawanga, Na Khadija Dalasia

Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Ndugu Msalika Makungu, amepokea ujumbe kutoka Wakala wa Nishati Vijijini (REA) uliokuja kutambulisha mradi mpya wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku.

Akizungumza wakati wa kutoa taarifa ya mradi huo, Mhandisi Kelvin Tarimo alisema kuwa zaidi ya shilingi milioni 291.3 zimetengwa kutekeleza mpango huo katika mikoa mbalimbali ya Tanzania Bara, ikiwemo Rukwa.

Kwa upande wa Rukwa, jumla ya majiko 5,094 yatasambazwa katika wilaya tatu za Kalambo, Sumbawanga na Nkasi, ambapo kila wilaya itapokea  majiko 1,698.

“Mradi huu unalenga kukuza upatikanaji wa nishati safi na endelevu, kupanua matumizi ya teknolojia za kisasa za kupikia na kupunguza utegemezi wa kuni na mkaa ambavyo vinachangia kwa kiasi kikubwa uchafuzi wa mazingira na afya,” alisema Mhandisi Tarimo.

Amesema kuwa REA imeandaa mpango wa kusambaza majiko banifu 200,000 kwa bei nafuu, ambapo gharama ya jiko moja bila ruzuku ni Shilingi 71,500, lakini kupitia ruzuku ya serikali ya asilimia 80, wananchi watanunua kwa bei ya Shilingi 14,300/=.

Akizungumza baada ya kupokea taarifa ya mradi huo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Ndugu Msalika Makungu, aliishukuru REA kwa kuunga mkono jitihada za serikali katika kuhakikisha ifikapo mwaka 2034, zaidi ya asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia.

Katika  Mkoa wa Rukwa, usambazaji na uuzaji  wa majiko banifu utafanywa na makampuni ya Greenway Grameen Infra Pvt Limited na ECOMANA Tanzania Limited.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE( CSEE) 2025 January 31, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO SUMBAWANGA; ASISITIZA UMUHIMU WA HATI MILIKI ZA MAENEO YA TAASISI

    January 29, 2026
  • UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO; RC MAKONGORO AHIMIZA UBORA NA KUZINGATIWA KWA MUDA WA UTEKELEZAJI NKASI DC

    January 28, 2026
  • KUMBUKIZI YA KUZALIWA RAIS SAMIA; RC MAKONGORO AMUUNGA MKONO KWA KUONGOZA WANANCHI RUKWA KUPANDA MITI 4565

    January 27, 2026
  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa