• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Rukwa wajipanga kutumia Mkaa mbadala kuokoa mazingira.

imewekwa Tar: October 26th, 2018

Mkoa wa Rukwa umejipanga kupambana na uharibifu wa mazingira kwa kuhakikisha wanatumia rasilimali za makaa ya mawe yanayopatikana katika kijiji cha Nkomolo tu, Wilayani Nkasi kuwa mkaa mbadala na kuanza kutumika majumbani.

Mkakati huo ulioanza kwa mafunzo ya siku mbili yaliyoendeshwa na mtaalamu wa makaa hayo kutoka katika ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe bi. Halima Mpita ukiwakutanisha makatibu tawala wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri, madiwani, wataalamu wa mazingira kutoka katika halmashauri, mashirika yasiyo ya kiserikali yanayoshughulikia mazingira pamoja na wazee maarufu.

Akiongea wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo ya nishati mbadala inayotokana na makaa ya mawe mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachima Wangabo amesema kuwa tunafanya kila liwekanalo kuokoa kile kilichopo na kuhakikisha kwamba mazingira hayaendelei kuharibiwa kwa namna yoyote hasa masuala ya kukata miti kwaajili ya kuni na mkaa.

“Makaa ya mawe yapo kilomita 45 toka hapa tulipo (sumbawanga mjini), yale makaa yam awe tunaweza kuyatumia kama mkaa mbadala kwa matumizi ya majumbani, na hili ndio lengo la mafunzo ya leo, mtaalamu wetu atatueleza kule Songwe wanafanyaje, kile wanachofanya kule watatumegea hapa uzoefu wao, na sisi tutaona na kujipanga tufanye nini na haya makaa yam awe tuliyonayo,” Alisema.

Ameongeza kuwa endapo mafanikio yatapatikana na kuanza kutumia makaa ya mawe majumbani, kiwango kikubwa cha uvunaji wa miti kitaokolewa na kutahadharisha kuwa mpango huo ukifanikiwa gharama za kununua bidhaa hiyo isiwakatishe tamaa wanunuzi ili wasirudi tena kukata miti na hatimae kutofikia lengo.

Kwa upande wake Bi. Mpita alisifu muitikio wa wadau wa mazingira wa mkoa wa Rukwa na kusema kuwa endapo nguvu hiyo itafikisha elimu kwa wananchi basi mkoa wa Rukwa utakuwa wa kuigwa na kuongeza kuwa atashirikiana bega kwa bega ili kuhakikisha mafanikio yanapatikana kwa faida ya kizazi hiki na kijacho.

Akieleza faida za mkaa unaozalishwa na makaa yam awe alisema, “Haya makaa ni suluhisho la kudumu juu ya matumizi mbadala la mkaa wa miti kwa kuwa miamba ya makaa ya mawe ni ya asili na inaweza kuvunwa zaidi ya miaka 500. Pia unaweza kuwaka kwa saa 3 hadi 4  mfululizo na hautoboi wala kuchafua sufuria, ni mkombozi wa ajira maana uanzishaji wa kiwanda chake ni rahisi na majivu yake hustawisha mimea,” Alisisitiza.

Ili kuuwasha Mkaa wa makaa ya mawe unahitaji jiko la mkaa lililotengenezwa kwa udongo, utawasha vijiti viwili maalum vya kuwashia moto utaweka vipande 4 hadi 5 acha viwake pamoja kwa dakika 3, ongeza mkaa na uache uko kwa dakia 15 hadi makaa ubadilike na kuwa rangi nyekundu kuanzia chini. Vipande 34 vya mkaa vinatosha kumaliza mapishi ambapo mkaa huo huwaka kwa masaa 3 hadi 4.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa