• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

imewekwa Tar: May 13th, 2025


Sumbawanga,13 Mei 2025.


Mkoa wa Rukwa umeanza rasmi utekelezaji wa mfumo wa stakabadhi ghalani. Katika hatua za awali, katika msimu wa Mwaka 2024/2025 mfumo huo utahusisha zao la mbaazi na ufuta.

Maelezo hayo yametolewa leo Mei 13, 2025 na Mheshimiwa Nyakia Ally Chirukile Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga alipomwakilisha Mheshimiwa Charles Makongoro Nyerere Mkuu wa Mkoa wa Rukwa katika kikao cha Maandalizi ya Msimu wa Masoko ya Mazao kwa Mwaka 2025/2026.


Mkuu huyo wa Wilaya ya Sumbawanga ameeleza kuwa hatua hiyo ya Serikali inalenga kusaidia wakulima kupata soko la uhakika la mazao na bei zenye tija.


Akifafanua juu ya matumizi ya mfumo huyo Mheshimiwa Chirukile ameeleza kuwa kuanzia msimu wa Mwaka 2024/2025, mazao ya mbaazi na ufuta hayatasafirishwa kutoka Halmashauri moja kwenda nyingine pasipo kuthibitisha kuwa yalipatikana kupitia minada ya kidigitali ya stakabadhi ghalani.


Ametoa mfano wa Mikoa ya Lindi na Ruvuma ambako mfumo huo umekuwa ukitumika na kuleta mafanikio. Amewahamasisha wakulima wa Mkoa wa Rukwa kuutumia mfumo huo kwa manufaa yao na sekta ya kilimo kwa ujumla.


Aidha Mheshimiwa Chirukile amewataka viongozi wa Halmashauri, Vyama vya Msingi (AMCOS), pamoja na taasisi wezeshi kama TMX, COPRA na WRRB kusimamia kikamilifu utekelezaji wa mfumo huo ili kuimarisha usimamizi wa soko na ubora wa mazao.

Kikao hicho kimefanyika katika Ukumbi wa RDC ulioko Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa na kuhudhuriwa na Wakuu wa Sehemu na Seksheni kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Kamati ya Usalama ya Mkoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Halmashauri, Vyama vya Ushirika na Taasisi Binafsi na Wakulima.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa