• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Sekta ya Afya Rukwa yatakiwa kuja na mikakati ya kumaliza matatizo ya uzazi

imewekwa Tar: June 5th, 2018

Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Benard Makali ameitaka sekta ya afya mkoani humo kuhakikisha wanaandaa mkakati wa kupunguza kama sio kumaliza kabisa tatizo la vifo vya watoto wachanga na akinamama vitokanavyo na matatizo ya uzazi.

Amesema kuwa mkakati huo utakamilika endapo kutakuwa na ufuatiliaji wa kila mwezi katika ngazi ya halmashauri pamoja na ufuatiliaji wa kila robo mwaka katika ngazi ya Mkoa ili kubaini changamoto mbalimbali zinazoibuka kila siku na kuona namna ya kuzitafutia ufumbuzi.

“Kwa mkoa wetu wa Rukwa, kwa mwaka 2017 kinamama 62 walipoteza maisha hii ni sawa na vifo 132 kati ya vizazi hai 100,000, na vifo vya watoto wachanga 15 kati ya vizazi hai 1,000. Kwa takwimu hizi hata kama tunaonekana tuna vifo vichache ikilinganishwa na viwango vya kitaifa bado sio nzuri, hivyo kuna kila sababu ya kuendelea kubuni na kutekeleza njia mbalimbali za kupunguza vifo hivi,” Alisema.

Aliyasema hayo alipokuwa akifungua kikao cha siku mbili cha kujadili vifo vya watoto wachanga na akinamama vitokanavyo na matatizo ya uzazi kilichowashirikisha wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri, waganga wakuu wa wilaya na timu za afya ngazi ya mkoa na wilaya.

Ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya tano inatekeleza haya kwa vitendo juhudi za kupunguza vifo hivyo kwa kuendesha zoezi la ukarabati na upanuzi wa vituo vyote vya afya nchini ambapo Mkoa wa Rukwa umepatiwa shilingi Bilioni 2.9 kukarabati na kujenga vituo vya afya 6 ambapo kazi hiyo inaendelea vizuri.

Kwa upande wake akisoma risala kbala ya kumkaribisha mgeni rasmi mratibu wa huduma ya afya na uzazi mkoa wa Rukwa Asha Izina amesema kuwa madhumuni ya mkoa ni kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo vitokanavyo na matatizo ya uzazi kwa wanawake na watoto chini ya umri wa miaka mitano na hasa wa chini ya mwaka mmoja na kuhakikisha makundi haya yanapata huduma muhimu Mkoa unatekeleza sera ya serikali ya kutoa huduma bila ya malipo.

“Katika kutekeleza maelekezo ya serikali, Mkoa kupitia ofisi ya mganga mkuu wa mkoa kwa kushirikiana na mradi wa UZAZI SALAMA Rukwa, tumeanza kufanya vikao vya kujadili vifo vya akinamama na watoto wachanga kila robo mwaka tangu mwanzoni mwa mwaka 2017 tukiwa na lengo la kuweka mikakati ya kukabiliana na vifo hivyo na hatimae kuokoa maisha ya akinamama na watoto wachanga,” Alisema.

Takwimu za mwaka 2015 – 2016 za utafiti wa viashiria vya huduma za afya na Malaria zinaonesha kuwa, vifo vitokanavyo na matatizo ya uzazi kitaifa ni 556 kwa kila vizazi hai 100,000 na vifo vya watoto wachanga ni 39 kwa kila vizazi hai 1,000.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa