• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Sekta ya Afya Rukwa yatakiwa kuja na mikakati ya kumaliza matatizo ya uzazi

imewekwa Tar: June 5th, 2018

Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Benard Makali ameitaka sekta ya afya mkoani humo kuhakikisha wanaandaa mkakati wa kupunguza kama sio kumaliza kabisa tatizo la vifo vya watoto wachanga na akinamama vitokanavyo na matatizo ya uzazi.

Amesema kuwa mkakati huo utakamilika endapo kutakuwa na ufuatiliaji wa kila mwezi katika ngazi ya halmashauri pamoja na ufuatiliaji wa kila robo mwaka katika ngazi ya Mkoa ili kubaini changamoto mbalimbali zinazoibuka kila siku na kuona namna ya kuzitafutia ufumbuzi.

“Kwa mkoa wetu wa Rukwa, kwa mwaka 2017 kinamama 62 walipoteza maisha hii ni sawa na vifo 132 kati ya vizazi hai 100,000, na vifo vya watoto wachanga 15 kati ya vizazi hai 1,000. Kwa takwimu hizi hata kama tunaonekana tuna vifo vichache ikilinganishwa na viwango vya kitaifa bado sio nzuri, hivyo kuna kila sababu ya kuendelea kubuni na kutekeleza njia mbalimbali za kupunguza vifo hivi,” Alisema.

Aliyasema hayo alipokuwa akifungua kikao cha siku mbili cha kujadili vifo vya watoto wachanga na akinamama vitokanavyo na matatizo ya uzazi kilichowashirikisha wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa halmashauri, waganga wakuu wa wilaya na timu za afya ngazi ya mkoa na wilaya.

Ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya tano inatekeleza haya kwa vitendo juhudi za kupunguza vifo hivyo kwa kuendesha zoezi la ukarabati na upanuzi wa vituo vyote vya afya nchini ambapo Mkoa wa Rukwa umepatiwa shilingi Bilioni 2.9 kukarabati na kujenga vituo vya afya 6 ambapo kazi hiyo inaendelea vizuri.

Kwa upande wake akisoma risala kbala ya kumkaribisha mgeni rasmi mratibu wa huduma ya afya na uzazi mkoa wa Rukwa Asha Izina amesema kuwa madhumuni ya mkoa ni kupunguza kwa kiasi kikubwa vifo vitokanavyo na matatizo ya uzazi kwa wanawake na watoto chini ya umri wa miaka mitano na hasa wa chini ya mwaka mmoja na kuhakikisha makundi haya yanapata huduma muhimu Mkoa unatekeleza sera ya serikali ya kutoa huduma bila ya malipo.

“Katika kutekeleza maelekezo ya serikali, Mkoa kupitia ofisi ya mganga mkuu wa mkoa kwa kushirikiana na mradi wa UZAZI SALAMA Rukwa, tumeanza kufanya vikao vya kujadili vifo vya akinamama na watoto wachanga kila robo mwaka tangu mwanzoni mwa mwaka 2017 tukiwa na lengo la kuweka mikakati ya kukabiliana na vifo hivyo na hatimae kuokoa maisha ya akinamama na watoto wachanga,” Alisema.

Takwimu za mwaka 2015 – 2016 za utafiti wa viashiria vya huduma za afya na Malaria zinaonesha kuwa, vifo vitokanavyo na matatizo ya uzazi kitaifa ni 556 kwa kila vizazi hai 100,000 na vifo vya watoto wachanga ni 39 kwa kila vizazi hai 1,000.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa