• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Serikali Mkoa wa Rukwa yawatahadharisha wananchi na Ugonjwa wa Ebola

imewekwa Tar: May 17th, 2017

Serikali ya Mkoa wa Rukwa imetoa tahadhari kwa wananchi kupitia kikao cha madiwani wa Halmashauri nne za Mkoa wa Rukwa kilichoitishwa na Sekretarieti ya Mkoa ili kupewa mafunzo ya kupitia taarifa za fedha na tathmini ya utekelezaji wa programu ya maboresho ya usimamizi wa fedha katika sekta ya umma awamu ya nne.

Tahadhari hiyo ilianza kutolewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen wakati alipokuwa akimalizia hotuba yake iliyolenga kuwaasa madiwani hao kuwa wasimamizi wa matumizi ya fedha katika Halmashauri zao na kuwafikishia ujumbe wa ugonjwa huo hatari wananchi katika kata wanazoziwakilisha.

Taarifa za Ugonjwa huo wa Ebola zimetolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto baada ya kupata taarifa kutoka “International Helath Regulation – National Focal Point” kuhusu mlipuko wa Ugonjwa wa Ebola katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) uliotangazwa na Shirika la Afya Duniani siku ya tarehe 12 Mei, 2017.

Ugonjwa wa Ebola umethibitishwa kwa kupitia vipimo vya maabara baada ya kutokea wagonjwa 9 ambpo kati yao 3 wamepoteza maisha na wengine 6 wanaendelea na matibabu katika kituo kilichoandaliwa. Ugonjwa huo umetokea katika jimbo la North – East Basuele, Afrika ya Kati.

“Ebola ni ugonjwa wa kumuomba Mungu apitishie mbali sana na Mkoa wa Rukwa, ni ugonjwa mbaya, Rukwa ni Mkoa wa Mpakani na dalili zake zimeshaanza kutokea kwa jirani zetu DRC, sasa wako wengine wanaotoka kwenye mitumbwi kwenye mialo yetu wanaopanda mabasi na wanaoleta biashara zao, pamoja na mambo mazuri mtakayokwenda kuyafanya ondokeni na hilo mkatoe tahadhari kwa wananchi,” Mh. Zelote alifafanua.

Nae kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Emanuel Mtika alipata nafasi ya kuelezea dalili anazopata mgonjwa ili kujua kuwa mgonjwa ameathirika na Ebola na kuongeza kuwa ugonjwa huo hauna tiba wala kinga na endapo utakupata kupona si rahisi.

“Miongoni mwa dalili zake ni homa kali ya ghafla, kulegea mwili, maumivu makali ya misuli, kuumwa kichwa na vidonda kooni, kuhara na kutapika na mara nyingine kutokwa na damu nyingi ndani na nje ya mwili na kujikinga kwake ni kumuepuka mgonjwa aliyeathirika na ugonjwa huo,” Dkt. Mtika alifafanua.

Nae Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa Tixon Nzunda kwa kulisisitiza hilo aliwakumbusha kuwa kinga ni bora kuliko tiba na kuweka wazi kuwa ugonjwa huo hauna tiba na kuwaasa walichukue jambo hilo na kulisambaza kuanzia kazi ya kijiji, hadi mtu kwa mtu.

“Tulichukue kama jambo la dharura na la kimkakati, tulifanyie kampeni kuanzia ngazi ya kijiji, kitongoji na tukienda mbali zaidi hadi ngazi ya mtu kwa mtu wa maana ya ngazi ya familia, tusisubiri yatukute,” Nzunda alibainisha.

Ugonjwa wa Ebola ni kati ya magonjwa yenye hatari ya kusambaa na kuleta madhara makubwa ya kiafya duniani, ingawa hadi sasa hapa nchini Tanzania hakuna mgonjwa yeyote aliyehisiwa ama kuthibitishwa kuwa ana virusi vya ugonjwa wa Ebola.

Matangazo

  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WAZAZI WAPATIENI WATOTO ELIMU KUHUSU HEDHI SALAMA

    June 02, 2023
  • WAWEKEZAJI KUTOKA ZAMBIA WAVUTIWA NA BANDARI MKOANI RUKWA

    May 28, 2023
  • MRADI WA MAJI WAZINDULIWA KISA

    May 15, 2023
  • ZAHANATI YA MPONA HALMASHAURI YA WILAYA YA SUMBAWANGA YAZINDULIWA

    May 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa