• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Japan Yatoa Msaada wa Vifaa Vya Upasuaji Rukwa vyenye thamani ya shilingi Milioni 139

imewekwa Tar: November 12th, 2019

SERIKALI ya Japani imetoa msaada wa vifaa vya upasuaji vyenye thamani ya shilingi milioni 139 katika wilaya za Kalambo na Nkasi mkoani Rukwa ambavyo vitasaidia akinamama wajawazito watakao kuwa wajifungua kwa njia ya upasuaji katika wilaya hizo.

Mashine hizo zimekabidhiwa katika kituo cha afya cha Mwimbi wilayani Kalambo na Balozi wa Japani nchini Tanzania, Takeda katshotoshi ambapo mashine hizo katika tarafa ya Mwimbi zitahudumia wakinamama waliopo katika vijiji 40.

Akikabidhi msaada huo balozi huyo, alisema kuwa mashine hizo zimetolewa msaada na serikali ya Japani kutokana na mahusiano mazuri yaliyopo baina ya nchi mbili ya Japani na Tanzania hivyo anaamini mashine hizo zitakuwa msaada kwa akina mama waliokuwa wanalazimika kusafiri umbali mrefu kwaajili ya kufuata huduma za upasuaji.

Naye Mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura, alisema kuwa msaada huo umetolewa na serikali ya Japani katika wakati muafaka ambapo hivi sasa serikali ya awamu ya tano imejikita katika kuboresha huduma za afya kwa kujenga majengo na kuweka vifaa tiba.

Alisema kuwa wanawake wanaoishi katika kata tisa, vijiji 40 wapatao 75,000 watakao hitaji huduma za upasuaji wakati wa kujifungua watapata huduma kwa kutumia mashine hizo zilizopo katika kituo cha afya cha Mwimbi.

Mkuu huyo wa wilaya alisema kuwa kabla ya kupatikana kwa mashine hizo baadhi ya wanawake waliokuwa wanahitaji huduma ya dharula ya upasuaji kwaajili ya kujifungua walikuwa wanalazimika kusafiri umbali wa kilometa 140 ili kufikia katika vituo vinavyotoa huduma za upasuaji.

Awali akisoma taarifa fupi kwa viongozi hao, mganga mfawidhi wa kituo cha afya Mwimbi Sospiter Mpuya, alisema kuwa tangu kituo hicho kimepokea mashine hizo mwezi April mwaka huu na kuanza kutoa huduma za upasuaji wanawake 62 wamefanyiwa upasuaji na kufanikiwa kupatikana watoto hai 61.

Alisema kuwa mtoto mmoja alipoteza maisha wakati huduma ikiendelea, lakini bila kuwepo kwa mashine hizo huenda idadi ya vifo vya wakina mama wanaohitaji huduma za upasuaji na watoto wanao zaliwa kwa njia ya upasuaji ingekuwa kubwa zaidi ya hiyo kutokana kukosekana huduma za upasuaji za dharula.

Naye kaimu mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kalambo Magreth Kakoya , alisema kuwa Halmashauri hiyo imetenga fedha kiasi cha shilingi milioni kumi kwaajili ya kuzifanyia matengenezo pindi zitakapo haribika ili kuhakikisha huduma hazo kotokosekana.

Pia aliwasihi wananchi kulipa Kodi hali itakayo iwezesha serikali kuboresha huduma za afya na nyinginezo kusaidia kupunguza changamoto zinazo wakabili.

Mmoja wa wanawake waliokuwepo katika hafla hiyo ya kukabidhi mashine hizo Joyce Sikazwe aliishukuru serikali ya Japani kwa kutambua kuwa wakina mama wa tarafa ya Mwimbi wilaya ya Kalambo kuwa wanahitaji mashine hizo ili waweze kuokoa maisha yao na watoto wao.

Aliwasihi wanawake wajawazito kuwa na tabia ya kuhudhuria kiliniki kitendo kitakacho wasaidia wataalamu wa afya kujua Kama wanahitaji huduma za upasuaji hali ambayo itachangia kuendelea kupunguza vifo vya wakina mama na watoto wilayani humo.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa