• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU TOZO ZA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO

imewekwa Tar: July 10th, 2025



Kalambo, Rukwa


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepiga marufuku kwa watumishi wa umma kuwaomba au kupokea malipo yoyote kutoka kwa wafugaji kwa ajili ya huduma za chanjo na utambuzi wa mifugo, ikiweka bayana kuwa huduma hizo zinatolewa bure kwa ufadhili wa Serikali.


Akizungumza Julai 8, 2025, katika Ranchi ya Taifa ya Kalambo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Edwin Mhede, alisema Serikali inalipa gharama zote za utekelezaji wa zoezi hilo kwa asilimia 100, na kuonya kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya mtumishi yeyote atakayebainika kukiuka agizo hilo.


"Zoezi hili ni la kitaifa, linaendeshwa kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alilizindua rasmi tarehe 16 Juni, 2025 huko Simiyu. Hakuna mfugaji anayepaswa kutozwa hata shilingi moja. Serikali inalipia kila kitu," alisema Dkt. Mhede.

Dkt. Mhede alibainisha kuwa katika mikoa ya Rukwa hususan wilaya za Nkasi na Kalambo, zoezi hilo linaendelea na tayari zaidi ya ng’ombe 1,500 kati ya zaidi ya 36,000 waliolengwa, wamekwishachanwa na kutambuliwa.


Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Ndugu Robert Msalika Makungu, alieleza kuwa mkoa huo unatarajia kuchanja zaidi ya ng’ombe 400,000 pamoja na mbuzi, kondoo na kuku, huku akisisitiza kuwa utaratibu wa ufuatiliaji umewekwa ili kuhakikisha utekelezaji unafanyika kwa haki, uwazi na ufanisi.


Baadhi ya wafugaji waliopatiwa huduma hiyo akiwemo Bi. Mgaya Myende wa kijiji cha Nkana na Bw. Benueli Makselo wa Sintali, walisema wamefurahishwa na zoezi hilo ambalo wamedai linapunguza gharama za matibabu ya mifugo, kuboresha afya ya wanyama wao, na kuongeza ulinzi kupitia heleni za utambuzi zinazotolewa bila malipo.

Zoezi la chanjo na utambuzi wa mifugo ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuboresha usimamizi wa mifugo nchini, kuongeza tija kwenye uzalishaji wa mazao ya mifugo, pamoja na kurahisisha upatikanaji wa takwimu sahihi kwa ajili ya kupanga maendeleo ya sekta hiyo.

Matangazo

  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2025 July 08, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA - 2025, KULINGANA NA MATOKEO YALIYOTANGAZWA NA BARAZA LA MITIHANI LA TAIFA (NECTA) June 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AFUNGUA JENGO JIPYA LA TAWI LA TCB SUMBAWANGA, APONGEZA KUIMARIKA KWA HUDUMA ZA KIFEDHA.

    July 10, 2025
  • UFAULU KIDATO CHA SITA; RUKWA YAZIDI KUPAA, RC MAKONGORO APONGEZA

    July 10, 2025
  • SERIKALI YAPIGA MARUFUKU TOZO ZA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO

    July 10, 2025
  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa