• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

SERIKALI YAPIGA MARUFUKU TOZO ZA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO

imewekwa Tar: July 10th, 2025



Kalambo, Rukwa


Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Wizara ya Mifugo na Uvuvi imepiga marufuku kwa watumishi wa umma kuwaomba au kupokea malipo yoyote kutoka kwa wafugaji kwa ajili ya huduma za chanjo na utambuzi wa mifugo, ikiweka bayana kuwa huduma hizo zinatolewa bure kwa ufadhili wa Serikali.


Akizungumza Julai 8, 2025, katika Ranchi ya Taifa ya Kalambo, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Edwin Mhede, alisema Serikali inalipa gharama zote za utekelezaji wa zoezi hilo kwa asilimia 100, na kuonya kuwa hatua kali zitachukuliwa dhidi ya mtumishi yeyote atakayebainika kukiuka agizo hilo.


"Zoezi hili ni la kitaifa, linaendeshwa kwa maelekezo ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye alilizindua rasmi tarehe 16 Juni, 2025 huko Simiyu. Hakuna mfugaji anayepaswa kutozwa hata shilingi moja. Serikali inalipia kila kitu," alisema Dkt. Mhede.

Dkt. Mhede alibainisha kuwa katika mikoa ya Rukwa hususan wilaya za Nkasi na Kalambo, zoezi hilo linaendelea na tayari zaidi ya ng’ombe 1,500 kati ya zaidi ya 36,000 waliolengwa, wamekwishachanwa na kutambuliwa.


Kwa upande wake, Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Ndugu Robert Msalika Makungu, alieleza kuwa mkoa huo unatarajia kuchanja zaidi ya ng’ombe 400,000 pamoja na mbuzi, kondoo na kuku, huku akisisitiza kuwa utaratibu wa ufuatiliaji umewekwa ili kuhakikisha utekelezaji unafanyika kwa haki, uwazi na ufanisi.


Baadhi ya wafugaji waliopatiwa huduma hiyo akiwemo Bi. Mgaya Myende wa kijiji cha Nkana na Bw. Benueli Makselo wa Sintali, walisema wamefurahishwa na zoezi hilo ambalo wamedai linapunguza gharama za matibabu ya mifugo, kuboresha afya ya wanyama wao, na kuongeza ulinzi kupitia heleni za utambuzi zinazotolewa bila malipo.

Zoezi la chanjo na utambuzi wa mifugo ni sehemu ya mkakati wa Serikali kuboresha usimamizi wa mifugo nchini, kuongeza tija kwenye uzalishaji wa mazao ya mifugo, pamoja na kurahisisha upatikanaji wa takwimu sahihi kwa ajili ya kupanga maendeleo ya sekta hiyo.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa