• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Shule siyo “Clinic” wala siyo “Maternity” – RC Rukwa

imewekwa Tar: July 19th, 2017


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen ameonya vikali wale wanaoendeleza gumzo la kuwatetea wanafunzi wanaopata mimba wakitaka warudishwe shule huku watoto wao wakiwa wanawalinda na kuhakikisha wanafanikiwa katika maisha.


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen akiongea na wanafunzi wa shule ya Sekondari Milundikwa juu ya kuachana na mapenzi shuleni na kuweka mbele masomo tu. 


Ameyasema hayo alipofanya ziara kujionea maandalizi ya mapokezi ya wanafunzi wa kidato cha tano katika shule mbili za Wilaya ya Nkasi kwa muhula wa mwaka 2017/2018, ambapo kwa Mkoa wa Rukwa wanafunzi 1,155 wamepangiwa kujiunga na shule 13 zinazochukua wanafunzi wa kidato cha Tano.

Mkuu wa Mkoa alisema kuwa kwa Mkoa wa Rukwa pekee kuna kesi 165 za wanafunzi kupata mimba tangu Januari hadi Juni mwaka huu na kesi zao zinaendelea kushughulikiwa ili kuwapata watuhumiwa na kuwachukulia hatua.

“Katika Mkoa wangu huu adui yangu namba moja ni yule ambae anampa mtoto wa kike mimba na yeyote anayetetea masuala yanayozunguka mimba, tusije tukaruhusu watu ambao wameshafanikiwa na watoto wao kielimu halafu wanakuwa kwenye majukwaa ya kuwaharibia watoto wa wazazi wengine, shule siyo Clinic wala siyo Maternity, wanafunzi hawaji shuleni kuapata mimba ni kusoma tu,” Mh. Zelote alisisitiza.



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen akikagua baadhi ya viti vya wanafunzi wa shule ya Sekondari Milundikwa akiwa pamoja naMkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda (wa tatu toka kulia)


Sambamba na hilo aliwataka wazazi wote kukemea vitendo hivi vinavyolenga kukatisha ndoto za wanafunzi hawa ambao wanaandaliwa kuijenga Tanzania ya viwanda, na kuongeza kuwa watoto ni wa watanzania si lazima awe wa kumzaa hivyo inampasa kila mzazi kuwa na uchungu pale anapoona mtoto wa mwenziwe amekatishwa ndoto zake kwa kupata mimba.

“Kwa wazazi na watu wazima hili lazima tulisimamie wote, mzazi, mtu mzima akimwona mtoto anafanya kitu kibaya achukue hatua, akemee na sio kupiga makofi na kutetea,” Alisema.

Katika kulisisitiza hilo Mh. Zelote aligawa nakala ya Marekebisho ya Sheria Mbalimbali Namba 2 ya mwaka 2016 ambayo katika kifungu 60A (1 – 4) imebainisha adhabu kwa watu wanaowapa mimba au kuoa ama kuolewa na mwanafunzi, kwa kifungo cha miaka 30 jela.

Awali akisoma taarifa fupi ya hali ya mimba katika Shule zilizopo Wilaya ya Nkasi Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Nkasi Abel Adam Ntupwa alisema kuwa wananchi na wazazi wengi hawaifahamu sharia ya elimu inayotaka mwanafunzi akipata mimba taarifa na vielelezo vinapelekwa kwa afisa mtendaji kata au Kijiji na kesi kupelekwa polisi kisha mahakamani.



Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen akiongea na mkandarasi wa Nyasa Drilling anayechimba kisima kwaajili ya Shule ya Sekondari Milundikwa, Wilayani Nkasi. 


“Baadhi ya wazazi na watendaji wanakula njama ya kutaka kumaliza kesi kienyeji kwa wazazi wa pande mbili kupatana, hivyo uongozi wa wilaya utatoa elimu pana juu ya haki ya msichana kusoma mpaka kumaliza na kuwachukulia hatua wale wanaosaidia kuficha wahalifu wa mimba,” Alisema.

Katika kuonesha umakini wa kulifuatilia suala hilo Afisa Elimu wa Mkoa wa Rukwa Robert Nestory alisisitiza kuwa upimwaji mimba kwa wanafunzi ufanywe mara kwa mara isiwe tu wakati shule zinapofunguliwa.

“Huu utaratibu wa kuwapima wanafunzi wakati shule zinapofunguliwa tuuache, upimwaji huu uwe ni wa mara kwa mara, na maafisa elimu wanapokwenda kutembelea shule mbali mmbali basi ni jukumu lao kuonana na wazazi ili wawape elimu ya sharia hii na sio tu kumuachia Mkuu wa Wilaya kazi hiyo,” Aliongeza.

Wakati akimkaribisha Mkuu wa Mkoa nae Mkuu wa Wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda alibainisha mpango wa kuwatangaza kwenye redio watuhumiwa wote ili jamii isikie na kuondoa dhana ya kuwaficha katika maeneo yao wanayoishi.

“Orodha yao watuhumiwa wote tunayo na redio tunayo, Nkasi FM, tutawangaza kwa majina ili wafamu kwamba wanatafutwa ili kuwatia hofu hasa maeneo ya huku vijijini,” Mh. Mtanda alimalizia.





Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa