• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

SIMBA SC YAICHAPA NAMUNGO FC MABAO 2-1 SUMBAWANGA NA KUTWAA TAJI LA TATU LA MSIMU

imewekwa Tar: August 2nd, 2020

KLABU ya Simba imehitimisha msimu wake mzuri baada ya kutwaa taji la tatu kufuatia kuichapa Namungo FC mabao 2-1 katika fainali ya Kombe la Shirikisho la Soka Tanzana (TFF), maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) jioni ya leo Uwanja wa Mandela, Sumbawanga mkoani Rukwa.


Simba SC ilifungua msimu vizuri kwa kubeba Ngao ya Jamii kwa ushindi wa 4-2 dhidi ya waliokuwa mabingwa wa ASFC, Azam FC Agosti 17, mwaka jana Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam na wiki mbili zilizopita ilitwaa ubingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara kwa mara ya tatu mfululizo.


Dalili za Simba kubeba taji lingine leo zilianza mapema tu dakika ya 27 baada ya nyota kutoka Msumbiji, Luis Jose Miquissone kufunga bao la kwanza akimalizia mpira uliookolewa na beki Carlos Protas kufuatia krosi ya beki wa kulia Shomari Salum Kapombe.

Na ni wakati huo Simba ilipata pigo kidogo, baada ya kiungo wake Mkenya, Francis Kahata Nyambura kushindwa kuendelea na mchezo kufuatia kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na mzawa, Hassan Dilunga aliyekwenda kuziba vyema pengo hilo.
Nahodha John Raphael Bocco akaifungia bao la pili Simba SC dakika ya 39 kwa kichwa cha kudundisha akimalizia pasi ya kichwa ya mchezaji wa zamani wa UD Songo ya kwao, Msumbiji Miquissone kufuatia krosi maridhawa ya kiungo Mzambia, Clatous Chotta Chama kutoka upande wa kulia.


Beki wa zamani wa Yanga SC, Edward Charles Manyama akaifungia Namungo FC bao la kufutia machozi dakika ya 56 akimalizia kona ya kiungo Abeid Athumani kutoka upande wa kulia.


Miquissone aliyesajiliwa msimu huu kutoka Mamelodi Sundowns ambayo ilimpeleka kwa mkopo klabu yake ya zamani, UD Songo alichaguliwa Mchezaji Bora wa Mechi baada ya mchezo huo Chama akachaguliwa Mchezaji Bora wa Mashindano.


Kikosi cha Simba SC kilikuwa; Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Kennedy Juma, Pascal Wawa, Jonas Mkude, Luis Miquissone, Gerson Fraga ‘Viera’, John Bocco, Clatous Chama na Francis Kahata/Hassan Dilunga dk27.


Namungo FC; Nourdine Balora, Rodgers Gabriel, Edward Manyama, Steven Duah, Carlos Protas, Hamisi Khalfan, Hashim Manyanya/Frank Mkumbo dk60, Daniel Joram/Steven Nzigamansabo dk46, Bigirimana Blaise, Lucas Kikoti na Abeid Athumani.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa