• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Stendi Kuu ya Mabasi Sumbawanga kufunguliwa mwezi Mei

imewekwa Tar: April 15th, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Sumbawanga kuhakikisha stendi kuu ya Mabasi iliyopo Katumba Azimio katika Manispaa hiyo kuwa inafunguliwa ifikapo tarehe 15.5.2021

Mh. Wangabo amesema kuwa awali Mkurugenzi huyo alitaka kuifungua stendi hiyo mwezi 29.1.2021 na kushindikana baada ya baadhi ya miundombinu kutokamilika vizuri na hivyo kuwaopa wiki moja kurekebisha miundombinu hiyo ndipo waifungue stendi hiyo tarehe 5.2.2021 na matokeo yake stendi hiyo haijafunguliwa hadi mwezi huu Aprili.

“Mpaka tarehe 15.5.2021 uwe umekamilisha kwa maana, ninyi ndio mliotaka kufungua siku moja kabla ya siku ile mi kufika (28.1.2021) halafu leo kuanzia mwezi ule wa pili, wa tatau, wa nne, unaongeza tena mwezi mwingine, imetoka wapi? Mkurugenzi fanya juu chini tarehe 15.5.2021 iwe mwisho, tunahitaji mapato pia, wananchi hawa wameeleza kero nyingi hapa zinahitaji fedha na fedha hizi zinatakiwa zitoke halmashauri sio kwa Mkuu wa mkoa,” Alisisitiza.

Mh. Wangabo alisema hayo (14.5.2021) katika hafla fupi ya kukabidhi hati kwa wananchi 13 wa Mtaa wa Sokolo baada ya zoezi la urasimishaji makazi katika mtaa huo kuisha na kuongeza kuwa kuwa ili changamoto za wananchi zitatuliwe halmashauri zinatakiwe zikusanye pesa kwa wingi na kutatua changamoto hizo na stendi hiyo ikikamilika ina uwezo wa kukusanaya karibu shilingi bilioni moja na hivyo kurahisisha mahitaji ya wananchi

Aidha katika hatua Nyingine Mtendaji mkuu wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Tanzania (ALAT) Elirehema Kaaya alipotembelea katika stendi hiyo tarehe 15.4.2021 katika ziara yake ya kutembelea miradi ya kimkakati iliyopo Manispaa ya Sumbawanga alisema kuwa ni vyema Manispaa hiyo ikazingatia maelekezo ya Mkuu wa Mkoa ili kuongeza mapato katika halmashauri.

“mkurugenzi ameniambia kwamba utayari wa wamiliki wa mabasi uko juu sana, wako tayari kuja wakati wowote hapa, kama alivyotoa maelekezo mkuu wa mkoa, kufikia tarehe 15.5.2021 wajitahidi kukamilisha ili kuhakikisha stendi hii inafanya kazi ili kukidhi madhumuni ya stendi hiyo ambayo ni kupunguza msongamano mjini pamoja na mapato, mimi nakijita kwenye mapato kwasababu ndio lengo kubwa, tupate mapato ambayo yatatusaidia kutoa huduma kwa wananchi,” Alisema.

Mapaka tarehe 15.4.2021 stendi hiyo imeshakamilika kwa asilimia 92 na kubakisha maeneo machache ikiwemo vibanda vya mama lishe na wafanayabiashara ambavyo vinaweza kuendelea kumaliziwa wakati stendi hiyo ikiendelea kufanya kazi.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa