• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

TARURA Rukwa Yasaini Mikataba

imewekwa Tar: November 1st, 2021



RC MKIRIKITI: BILIONI 12 KUTEKELEZA MIRADI YA TARURA.

Wakandarasi wanaofanya kazi ya kutekeleza miradi chini ya Wakala wa Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwenye mkoa wa Rukwa wametakiwa kuzingatia nidhamu ya kazi ili miradi iwe bora na endelevu.

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti ametoa agizo hilo leo (01.11.2021) wakati wa kikao cha kazi na wakandarasi wanaotekeleza miradi mbalimbali chini ya Tarura kwa mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga.

Mkirikiti ameonya tabia iliyoanza kujengeka miongoni mwa wakandarasi kuona miradi hiyo siyo ya kipaumbele wakati inatumia fedha nyingi za walipakodi wa Tanzania.

“Nidhamu kwenye utendaji kazi wa wakandarasi ni jambo muhimu ili fedha zinazotolewa na serikali kupitia TARURA zitumike kwa ufanisi na kuleta matokeo chanya ya ubora wa miradi ya barabara zetu. Nataka kuona mkoa huu wakandarasi mnaheshimu mikataba yenu ya kazi,” alisisitiza Mkirikiti.

Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni kikao chake cha kwanza na wakandarasi wa miradi ya barabara aliwafahamisha kuwa tayari serikali imekwisha toa shilingi Bilioni 12 kwa ajili miradi 49 kote kwenye halmashauri chini ya Tarura katika kipindi cha mwaka huu.

Mkirikiti alitumia pia kikao hicho kutoa onyo kwa wahandisi wa TARURA kwenye halmashauri za mkoa wa Rukwa kuacha tabia ya kutoa kazi kwa wakandarasi wasio na sifa na uwezo wa kutekeleza miradi hatua inayorudisha nyuma jitihada za serikali.

Kwa upande wake Meneja wa TARURA Mkoa wa Rukwa Mhandisi Seth Mwakyembe alisema katika kikao hicho jumla ya mikataba ya ujenzi 16 yenye thamani ya shilingi Bilioni 4.5 ikiwa ni sehemu ya Shilingi Bilioni 12 itasainiwa baada ya uchambuzi wa kina kujiridhisha na sifa za wakandarasi.

Mwakyembe alimfahamisha Mkuu wa Mkoa kuwa, Tarura imejipanga kuhakikisha miradi hii itakayosainiwa licha ya kuwa ni kipindi cha mvua kukaribia itakwenda kutekelezwa kwa kasi na kwa ubora ili kutatua changamoto za barabara hususan vijijini.

“Tarura inatoa pongezi kwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kutambua umuhimu wa kuboresha barabara za mjini na vijijini ambako watanzania wana uhitaji wa miundombinu bora. Tutasimia fedha hizi zilete tija” alisema Mhandisi Mwakyembe.

Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya JEMO Mary Obadia Mbwilo akizungumza kwa niaba ya wakandarasi wa Rukwa alisema anaishukuru serikali kwa kutoa kipaumbele cha kazi kwa wakandarasi wa Rukwa wakiwemo wanawake hatua inayosaidia wakuze uwezo wao wa kazi na uchumi.

Mdau huyo alibainisha kuwa “tupo wakandarasi wanawake wanne(4) tuliopata kazi msimu huu, hatutawaangusha tutatekeleza kazi kwa ubora ili siku za mbele wanawake zaidi wenye ujuzi na uwezo waweze kupata mikataba ya kazi TARURA” alihitimisha Mbwilo.

Kwa upande wake Mkuu wa TAKUKURU Mkoa wa Rukwa Daniel Ntera akitoa mada kwa wakandarasi hao amewataka wazingatie mikataba yao ya kazi na kutojishusisha na vitendo vitakavyohujumu ubora wa miradi.

Ntera aliwafahamisha kuwa Takukuru inafuatilia kwa karibu kazi zote za wakandarasi ili kudhibiti mianya ya rushwa hatua itakayosaidia miradi iwe bora na fedha za umma zitumike kwa kazi zilizopangwa kwenye mikataba.

Mwisho.


Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa