• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

TARURA watakiwa kushughulikia maeneo korofi msimu wa mvua

imewekwa Tar: November 30th, 2019

Wakala wa Barabara za mijini na Vijijini (TARURA) wametakiwa kuhakikisha Barabara zote za Vijijini zinapitika mwaka Mzima kwa kufanyiwa matengenezo na endapo itashindikana basi ni muhimu kuyapa kipaumbelea maeneo korofi, hasa katika kipindi hiki cha Mvua jambo ambalo litawasaidia wananchi kuendelea na shughuli zao za Kiuchumi bila vikwazo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo katika kikao cha Bodi ya barabara baada ya wabunge wa mkoa huo pamoja na wenyeviti wa halmashauri kuilalamikia TARURA juu ya utendaji wake wa kazi pamoja na mipangilio yao ya bajeti katika kutekeleza majukumu yao.

“Wakala wa Barabara za Vijijini (TARURA) kuhakiki Barabara zote za vijijini katika Halmashauri zote za Mkoa wa Rukwa ili kwanza wawe na orodha kamili ya Barabara za Vijijini na  zipo kwenye hali gani,Baada ya kuhakiki wawe na orodha ya Barabara zilizoingizwa kwenye Mtandao wa  Barabara za TARURA na Barabara zipi hazipo kwenye mtandao wa Barabara za TARURA na kwanini?,” Alihoji

Aidha alisema kuwa kwa kufanya hivyo itawasaidia TARURA kuwa na picha ya Barabara zote za Mkoa wakati wa upangaji wa Bajeti ya mwaka 2020/2021 ili waweze  kuziweka kwenye Bajeti Barabara ambazo zinahitaji Matengenezo.

Wakati wakiwasilisha malalamiko hayo miongoni mwa wabunge hao walisema kuwa hawaridhishwi na bajeti inayotengwa na TARURA na hata hiyo inayotengwa haifikishwi kwa wakati hali ambayo inasababisha hata hicho kidogo kilichotengwa kushindwa kufanya kazi iliyokusudiwa.

Mbunge wa Nkasi Kaskazini Mh. Ali Kessy alisema, “Tumepanga bajeti milioni 400 wazilete zote milioni 400, hauwezi kupanga bajeti milioni 400 unaleta milioni 20, nimemuuliza mratibu wa (TARURA) Mkoa, mmeleta shilingi ngapi anasema tumeleta milioni 20 kwenye bajeti ya serikali ya milioni 400, walitenga kabia daraja la Kavunje, wakadarasai wamekwama daraja haliendelei na mvua ndio hiyo kama unavyoona.”

Naye Mbunge wa Nkasi Kusini Mh. Desderius Mipata alisema kuwa wananchi wa kata ya Ninde watatengwa kutokana na TARURA kushindwa kutenga bajeti kwaajili ya ukarabati wa barabara inayowaunganisha wananchi wa kata hiyo na kata za jirani.

“Kwahiyo naomba mtafute njia yoyote ya dharura ya kuwezesha eneo hilo lipitike hakuna namna nyingine ya kufanya, nikiwa bungeni daraja la kwenda ninde lilikuwa limevunjika, nikapiga kelele bahati nzuri walikuja wakatengeneza kwa pesa kidogo lakini barabara yake haipitiki,” Alimalizia.

Wakati akitoa malalamiko yake kwa niaba ya wakandarasi wenzie Bwana Anyosisye Kiluswa amesema kuwa wakandarasi bado wanazidai halmashauri fedha za matengenezo ya barabara kadhaa kabla ya barabara hizo hazijahamishiwa kwa TARURA na kuongeza kuwa halmashauri hizo zilishapewa fedha na serikali lakini matokeo yake wametumia kwa matumizi mengine.

“Sasa kwa sasa hivi wakandarasi tunashindwa kutekeleza wajibu wa kufanya kazi kwasababu pesa zetu wenyewe ni za kuunga unga, ukifanya kazi umelipwa halafu pesa hiyo hiyo unaichukua unakwenda kufanya kazi sehemu nyingine, sasa unapokuwa unafanya kazi bila ya kulipwa na nyingine ambazo zipo wanazitumia kwenye maeneo mengine matokeo yake wakandarasi wa mkoa wa Rukwa tunaonekana hatufanyi kazi vizuri,” Alisisitiza.

Kwa upande wake Kaimu mratibu wa TARURA Mkoa wa Rukwa alisema kuwa kwa mwaka wa fedha 2019/2020 jumla ya fedha shilingi bilioni 4.133 kwaajili ya matengenezo ya barabara km 346.63 na vivuko 48 huku kutoka mfuko wa barabara zikitengwa shilingi bilioni 1.763 kwaajili ya miradi ya maendeleo ambapo daraja la mto Kavunja likitengewa shilingi milioni 400 na daraja la mto Kanteza lilopo Laela likitengewa shilingi milioni 163.2.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa