• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

TASAF

imewekwa Tar: February 5th, 2023

TASAF IFUNDISHE STADI ZA KUKUZA KIPATO - RC SENDIGA

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga ameagiza wataalam wanaosimamia Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) katika ngazi ya halmashauri kuwafundisha wanufaika stadi za kazi zitakazosaidia kuinua kipato cha wananchi.

Ametoa kauli hiyo ( Februari 04,2023) wakati kukagua kikundi cha wanufaika wa TASAF waliopo kijiji cha Ilemba Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga wanaojishughulisha na mradi wa miti ya matunda na mbao.

“Wafundisheni wanufaika hawa kuwa na miradi yao ya mashamba ya miti au ufugaji mifugo katika kaya zao ili kipato kidogo wakipatacho toka serikalini kiwe ni mtaji wa kukuza uchumi . Wafikirie kubuni miradi siyo kutegemea fedha za TASAF” alisema Sendiga.

Sendiga aliongeza kusema fedha wanazopata wanufaika siyo fungu la mirathi na kuwa wasipewe kama sadaka bali wafundishwe ujasiliamali wa kuwa na miradi yao ili siku serikali ikisitisha programu hiyo waweze kujitegemea.

Nao wanufaika wa TASAF toka kijiji cha Ilemba waliozungumza na mwandishi wetu walikuwa na haya ya kusema ,Everada Kapaya alisema amenufaika na mfuko wa Tasaf tangu mwaka 2015 ambapo ameweza kujenga nyumba ya vyumba viwili na kusomesha watoto wake wanne pamoja na kuanzisha ufugaji wa ng’ombe mmoja .

Evarada alisema ‘nashukuru serikali kwa mradi huu wa Tasaf na ninaomba Rais Samia Suluhu Hassan aendelee kutusaidia ili tuweze kusomesha watoto wapate elimu nzuri” .

Naye Elizabeth Pesambili mkazi wa Ilemba alisema kupitia mfuko wa Tasaf ameweza kulea wajukuu zake 16 ambao aliachiwa na watoto wake  na kuwa sasa ana miaka mitano akipata pesa toka serikalini.

Katika hatua nyingine Mkuu wa Mkoa huyo wa Rukwa alikagua miradi ya ujenzi wa zahanati kijiji cha Muze, Uzia, Hospitali ya Wilaya Mtowisa pamoja na shule za sekondari Mazoka na Ilemba .

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Jane Nyamsenda akizungumza kwenye ziara hiyo alisema atahakikisha anashirikiana na wananchi wa Sumbawanga kutekeleza miradi yote iliyopo na kubuni mingine kwa ustawi wa jamii.

Mwisho.

Matangazo

  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • JAMII ISHIRIKIANE NA WALIMU KUKUZA TAALUMA

    February 16, 2023
  • Kampeni Upandaji Miti

    February 07, 2023
  • TASAF

    February 05, 2023
  • RAS Mchatta akagua miradi

    January 26, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa