• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Timu ya Tanzania Prisons yapokewa Kifalme Sumbawanga huku wakiombewa kushinda mechi zote za ligi

imewekwa Tar: August 22nd, 2020

Wadau mbalimbali wa michezo katika mji wa Sumbwanga wamejitokeza kwa wingi kuipa mapokezi ya aina yake timu ya jeshi la Magereza Tanzania – Tanzania Prisons ambayo imethibitisha kuutumia uwanja wa Nelson Mandela Mkoani Rukwa kama uwanja wake wa nyumbani katika msimu wa 2020/2021 wa Ligi Kuu Bara jambo ambalo lilikuwa likisubiriwa kwa hamu na wananchi wa mkoa huo ili kupata burudani ya michezo waliyoikosa kwa zaidi ya miaka 23.

Juhudi hizo za kufanikisha timu hiyo kuweka makazi yake katika mkoa huo ni ushawishi mkubwa uliofanywa na mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh.Joachim Wangabo pamoja na uongozi wa mkoa huo huku akiungwa mkono na wadau wa michezo mkoani humo baada ya kuona faida kubwa iliyopatikana kutokana baada ya fainali za kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) kufanyika katika uwanja huo uliokarabatiwa kwa kiwango cha hali ya juu.

Wakati akizungumza baada ya kamanda wa Jeshi la magereza mkoa wa Mbeya kuikabidhi timu hiyo kwa kamanda wa Jeshi la Magereza Mkoa wa Rukwa Mh. Wangabo alisema kuwa ndoto waliyokuwa wakiiota sasa imegeuka kweli baada ya timu hiyo kutua rasmi katika mkoa na wananchi kuishuhudia ikiingia katika uwanja wa Nelson Mandela ambao utatumika katika mechi zao za Ligi Kuu.

“Timu hii imekuja wakati muafaka, tumekuwa hatuna timu katika ligi daraja la kwanza, daraja la pili, mpaka huko ligi kuu hatuna kwa miaka mingi sana, zaidi ya robo karne, hatuna timu kwahiyo na wananchi wamekosa burudani hii, na hawa watu wote hawa unaowaona hapa wamekuja wanapenda michezo, sisi tulikuwa tuna deni kubwa kama viongozi, tunaongoza wananchi ambao tunawanyima furaha, sasa tumeamua kuwapa furaha wanarukwa wote pamoja na wa mikoa ya jirani,” alisema.

Aidha, Ameiombea timu hiyo kushinda michezo yake yote miwili ya ugenini ambayo wanaanza na timu ya Young Africans SC pamoja na KMC FC katika jiji la Dar es salaam na kufuatiwa na mechi za za Nyumbani wataanza na Namungo FC, Azam FC pamoja na Simba SC zitakazochezwa katika Uwanja huo wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga.

“Mwezi wa kumi tunacheza na Simba SC ya Dar es Salaam, sasa siku hiyo, nilisema hizi timu nyingine zisione zitafute mpira kwa tochi, hawa Simba ndio wasiuone kabisaaa, mpaka waulize hivi goli liko wapi, pengine goli liwe hili benchi la ufundi, yaani nasema wasione mpira kwa namna mtakavyotandaza mpira hapa, pasi fupi fupi na ndefu muwachanganye kabisa mpaka wapoteane hapa,” Alisisitiza.

Katika mapokezi hayo MH. Wangabo aliikabidhi timu hiyo Seti ya jezi pamoja na mipira kwaajili ya maandalizi yao kuelekea kuanza kwa ligi hiyo tarehe 6.8.2020 huku kamati maalum inayoshughulikia ustawi wa wachezaji wa timu hiyo ikiongozwa na Mzee Dkt. Chrisant Majiyatanga Mzindakaya wakitoa chakula kwa wachezaji pamoja na ng’ombe mmoja

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa