• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

TMDA na Udhibiti wa Tumbaku

imewekwa Tar: December 15th, 2021

TMDA YATOA ELIMU KWA UMMA KUHUSU UDHIBITI WA TUMBAKU RUKWA

Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA) Kanda ya Nyanda za Juu Kusini imepongezwa kwa kutoa elimu juu ya matumizi na athari za tumbaku na mazao yake kwa wananchi wa mkoa wa Rukwa hususan Vijijini.

Pongezi hizo zimetolewa leo (15.12.2021) na Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Denis Bandisa wakati wa kikao chake na Maafisa wa TMDA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini yenye makao makuu yake Mbeya waliofika ofisini kwake Sumbawanga  kuelezea  kazi ya uelimishaji umma juu ya majukumu ya TMDA katika udhibiti wa tumbaku kwenye wilaya za Rukwa.

“Ninawapongeza kwa kufika maeneo mengi ya pembezoni huko vijijini ambapo kuna watu wengi na kuwapa elimu juu ya athari za matumizi ya tumbaku kwa afya zao ili wachukue hatua za kufanya maamuzi sahihi” alisema Bandisa

Katibu Tawala huyo wa Mkoa aliwataka Maafisa hao wa TMDA kujitahidi kufika kwenye maeneo yenye watu wengi zaidi Vijijini na kutoa elimu ya shughuli za Mamlaka hiyo muhimu katika kudhibiti matumizi yasiyo sahihi ya dawa na vifaa tiba ikizingatiwa kuwa mkoa wa Rukwa upo mipakani na nchi za DRC Congo na Zambia

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TMDA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Anitha Mshighati alieleza kuwa tayari wamefanikiwa kufika katika wilaya za Nkasi, Kalambo na Sumbawanga ambapo wametoa elimu kwa wajumbe wa kamati za maendeleo ya kata nne kila halmashauri.

Mshighati alitaja mafanikio mengine kwenye zoezi hili kuwa wametoa elimu juu ya majukumu ya TMDA na athari za tumbaku kwa vyuo vya Waganga St. Bakita cha Nkasi pamoja na Chuo cha Waganga Sumbawanga.

“Tupo hapa Rukwa tangu Desemba 08 mwaka huu tukitoa elimu kwa umma juu ya madhara ya tumbaku na namna ya kukabiliana nayo ikiwa ni jukumu la Mamlaka yetu TMDA kuelimisha wananchi “alisema Mshighati.

Mtaalam huyo wa dawa alisema katika kazi hiyo wamepata wasaa wa kuongea na wananchi kwenye vikao vya kata nyingi ambapo wamebaini kuwa bado kuna uhitaji mkubwa wa elimu kwa wananchi juu ya athari za matumizi ya bidhaa za tumbaku.

Wataalam hao wa TMDA pia leo wameshiriki kutoa elimu athari za tumbaku kupitia redio Chemchem FM na Ndingala FM za mjini Sumbawanga ambapo wananchi walipata fursa ya kuuliza maswali na kujibiwa.

Kesho wataendelea na kazi ya kutoa elimu ya udhibiti tumbaku na mazao yake kwa kamati za maendeleo za kata za Mwadui, Muze, Mkwawa na Ikozi zilizopo Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga.

Mwisho.

Matangazo

  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Kodi kwa Maendeleo September 15, 2021
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Chanjo Polio

    May 18, 2022
  • NFRA

    May 11, 2022
  • Vyama vya Ushirika

    May 05, 2022
  • Eng. Kundo: Nimeridhishwa na Zoezi la Anwani za Makazi Rukwa

    April 27, 2022
  • Angalia Zote

Video

RC Mkirikiti akabidhiwa Ofisi Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0764902066

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa