• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Udhibiti wa Dawa na Vifaa Tiba

imewekwa Tar: September 15th, 2021

RC MKIRIKITI: TMDA ELIMISHENI VIONGOZI WA VIJIJI KUDHIBITI MADAWA NA VIFAA TIBA MIPAKANI


Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) imeshauriwa kuelimisha na kuwatumia viongozi wa vijiji na tarafa hususan waliopo mipakani kudhibiti uingizwaji wa vifaa tiba na madawa yasiyo na ubora toka nje ya nchi visisambae mkoani Rukwa.

Kauli hiyo imetolewa  na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Joseph Mkirikiti wakati alipokutana ofisini kwake na wataalam wa TMDA Nyanda za Juu Kusini toka Mbeya leo (15.09.2021) mjini Sumbawanga ambao wapo mkoani Rukwa kwa kazi ya ukaguzi wa madawa na vifaa tiba kwenye halmashauri .

“Tumieni uwepo wa mifumo ya kiutendaji ya serikali iliyopo kuanzia vijiji na tarafa hususan kwenye mipaka yetu na nchi za jirani ambako kwa uchunguzi wenu ndiko vifaa tiba na madawa mengi yasiyo na ubora hupitia kuingia nchini ikiwemo kwenye mkoa wa Rukwa” alisema Mkirikiti.

Mkirikiti amewakaribisha wataalam hao kuandaa taarifa ya hali ya uingiaji vifaa tiba na madawa yasiyo na ubora ikiwemo mikakati yao ya kudhibiti ili kuikinga jamii na matumizi yasiyo sahihi ya bidhaa hizo ambapo wataweza kuwasilisha kwenye kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) mwezi ujao.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Nyanda za Juu Kusini Anitha Mshighati alisema tatizo la uingizwaji vifaa tiba na madawa yasiyokidhi viwango ni kubwa kwenye maeneo ya mpakani na nchi za Congo na Burundi .

Aliongeza kusema jitihada za mamlaka ni kuendelea kuzishi Mamlaka za serikali za mitaa mkoani Rukwa kushirikiana na TMDA ili kudhibiti uingizwaji wa madawa kinyume cha taratibu za nchi.

“Katika ukaguzi wetu wa mwezi Agosti mwaka huu tumebaini bado changamoto ya dawa na vifaa tiba kuingizwa nchini kinyemela kwenye mipaka ya mkoa wa Rukwa na nchi za jirani husuan Ziwa Tanganyika. Tunaomba mkoa usaidie udhibiti wake kwa kutumia vyombo vya dola” alisema Anitha.

Katika hatua nyingine Anitha  alimhakikishia Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kuwa wataalam wa TMDA wataendelea kushirikiana na Viongozi wa chama na Serikali katika kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya dawa na vifaa tiba vyenye kuzingatia ubora na vilivyothibitishwa na TMDA ili kulinda afya za watanzania na uchumi wa nchi.

 Mwisho

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa