• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Udhibiti wa Kipindupindu

imewekwa Tar: September 28th, 2022

SERIKALI KUDHIBITI UGONJWA WA KIPINDUPINDU - DKT.MNKENI

Na. OMM Rukwa

Afisa Mpango wa Taifa wa Afya Shuleni toka Wizara ya Afya Dkt. Emmanuel Mnkeni amesema serikali itaendelea kuchukua hatua kudhibiti mlipuko wa magonjwa ikiwemo kipindupindu.

Dkt. Mnkeni alisema mafunzo kwa Wahudumu wa Afya ngazi ya Jamii ( CHWs), Walimu na Wenyeviti wa kamati za Shule yanalenga kuhamasisha jamii kuhusu ujenzi wa vyoo bora na usafi wa mazingira ili kudhubiti magonjwa ya mlipuko ikiwemo kipindupindu.

Mafunzo hayo yametolewa leo ( 27.09.2022) katika kijiji cha Kirando Wilaya ya Nkasi ambapo Wizara ya Afya inalenga kuhamasisha na kuelimisha viongozi na jamii kushirikiana ili kuweka utamaduni wa kutumia vyoo bora.

" Wizara ya Afya kwa kushirikana na OR- TAMISEMI inaendelea kutoa elimu endelevu ili jamii iweze kubadilika kwa kutumia vyoo bora,kunawa mikono kwa maji tiririka pamoja na kunywa maji safi na salama" alisema Dkt. Mnkeni.

Kwa upande wake Peter Muna ambaye ni Mwenyekiti wa Kamati ya Shule ya Msingi Mkinga alisema Sheria ndogo ziendelee kutumika hata pale ugonjwa wa kipindupindu unapoisha na kuwa viongozi wa vijiji wawe mfano wa kuigwa kwa kuwa na vyoo safi na kuvitumia.

Naye Mwalimu Betty Sungura toka Shule ya Msingi Mpata kata ya Kirando aliiomba serikali iongeze nguvu katika upatikanaji wa miundombinu ya kutosha ya matundu ya vyoo ili watoto waepuke mlundikano wanapoenda chooni.

" Miundombinu mibovu ya vyoo kinakuwa chanjo cha mlipuko wa magonjwa hususan pale shule inapokuwa na msongamano wa watoto" alisema Mwalimu Sungura.

Kwa upande wake Afisa Elimu ya Msingi Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Augustine Bayo alibainisha kuwa viongozi wa vijiji na kata ndio wenye jukumu la kuhakikisha wanafunzi wakuwa na vyoo bora na vinatumika .

Bayo aliongeza kusema serikali inajitahidi kutenga fedha za kuwezesha ujenzi wa miundombinu ya vyoo kupitia mradi wa SWASH.

"Kila kaya au shule lazima iwe na vyoo bora ili kudhibiti mlipuko wa magonjwa ikiwemo kipindupindu " alisema Bayo.

Wilaya za Nkasi na Kalambo kwa nyakati tofauti zimekuwa na mlipuko wa ugonjwa wa kipindupindu.

Kipindupindu ni ugonjwa wa kuharisha na kutapika unaosababishwa na vimelea vya bakteria vinavyoitwa kwa lugha ya kitaalam " Vibrio cholera" na madhara yake ni pamoja na vifo.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa