• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Ujenzi wa Vymumba vya Madarasa kuwa agenda ya kudumu mkoani Rukwa

imewekwa Tar: December 18th, 2020

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaagiza Wakurugenzi wa Halmashauri kuhakikisha kuwa Suala la ujenzi wa madarasa linakuwa agenda ya kudumu katika vikao vyote vya kisheria vya halmashauri kwakuwa idadi ya wanafunzi wanaoandikishwa kujiunga na shule imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.

Amesema kuwa mbali na ujenzi huo wa madarasa mkoa una jumla ya kata 27 ambazo hazina shule za sekondari na hivyo kuwaagiza Wakuu wa Wilaya na Wakurugenzi kuhakikisha kuwa kata hizo zinakuwa na shule za Sekondari hata ikibidi kuanza kwa ujenzi wa madarasa manne ili ifikapo mwaka 2022 madarasa hayo yaweze kuchukua wanafunzi 200 katika shule hizo mpya.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani humo kushiriki katika jitihada mbalimbali za ujenzi wa miundombinu ya shule kwa lengo la kuboresha mazingira ya shule na kukumbusha kuwa ushiriki wa shughuli za maendeleo ni jukumu la kila mwananchi.

“Ndugu wajumbe hatuwezi kwenda kwa zimamoto, kila ifikapo mwishoni mwa mwaka tunaanza maagizo kama haya, hakuna likizo, hakuna nini, kamata kamata sijui nini, mkurugenzi ujenge vyumba vya madarasa kuna upungufu kama vile hatujui, tunafahamu kwamba tunayo changamoto ya vyumba vya madarasa kwa kila halmashauri, sasa ni jukumu letu sisi viongozi kuhakikisha kwamba hatuendi kwa ‘pressure’ tunajipanga tangu mwanzoni mwa mwaka mpaka mwisho,” Alisisitiza.

Halikadhalika alisema,” Naagiza Wazazi na Walezi kuhakisha Wanafunzi waliochaguliwa wanaripoti kwa asilimia 100 katika shule walizopangiwa na kwa mujibu wa ratiba ya kufungua Shule tarehe 11 Januari, 2021 na katika hili Wakuu wa Wilaya wachukue hatua kali kwa Wazazi watakaoshindwa kuhakikisha vijana wao wanaripoti katika shule walizopangiwa kwa kuwafikisha katika vyombo vya Sheria.”

Kwa upande wake Kaimu Afisa Elimu Mkoa wa Rukwa William Mwaisumo alisema kuwa baadhi ya changamoto zinazokwamisha maendeleo ya taaluma mkoani humo ni Pamoja na baadhi ya wazazi ama walezi kutosimamia ipasavyo watoto wao baada ya kuhitimu Darasa la Saba hivyo baadhi ya watoto kutoripoti kutokana kupata mimba au baadhi yao kupelekwa kufanya kazi mashambani, majumbani au machungani.

“Tafsiri potofu ya dhana ya Elimu bila Malipo hii hupelekea baadhi ya wazazi kutoshiriki kikamilifu katika shughuli za maendeleo ya shule, na wengine kutokuwajibika kikamilifu katika usimamizi wa watoto wao hasa kuwapatia mahitaji muhimu ikiwemo mahitaji ya shule na chakula hivyo Jamii wanatakiwa kuelewa dhana ya Elimu bila Malipo kuwa haindoi wajibu wa wazazi na wanajamii kushiriki kwenye masuala ya maendeleo ya shule na haindoi wajibu wa wazazi kwa watoto wao ikiwemo suala la kuwapatia mahitaji muhimu ikiwemo chakula,” Alisema.

Wakati akitoa neno la Shukurani Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi Mh. Pancras Maliyatabu alisema kuwa kama viongozi wa kisisasa watajitahidi kuwaelekeza wazazi kuwatimizia Watoto wao mahitaji ya msingi ili waendelee kufanya vizuri katika masomo yao.

“Lakini Katika ujenzi wa upungufu wa vyoo na madarasa tutaendelea kuwaelimisha wananchi juu ya kujitolea nguvu zao ili baadae serikali ije ijazie kumalizia ujenzi wa madarasa ili kutengeneza mazingira mazuri uya Watoto kusomea,” Alisema.

Wanafunzi 16,540 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mkoani Rukwa kati ya wanafunzi 17,104 waliofaulu mtihani huo wa kumaliza Elimu ya Msingi huku wanafunzi 564 wakikosa nafasi katika awamu hii ya kwanza baada ya Mkoa kuwa na upungufu wa madarasa 14 katika halmashauri ya Wialaya ya Kalambo na Manispaa ya Sumbawanga ambayo yanatakiwa kukamilika kabla ya tarehe 28.2.2021.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa