• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

“Ushiriki wa Kinababa ni muhimu katika wiki ya Unyonyeshaji” RC Wangabo.

imewekwa Tar: July 31st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi wa mkoa wa Rukwa hasa kinababa kushiriki katika maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji yanayofanyika kila mwaka kuanzia tarehe 1 hadi 7 ya Mwezi wa Nane ambapo Tanzania huungana na nchi nyingine duniani katika maadhimisho hayo.

Amesema kuwa wiki hiyo ya unyonyeshaji itumike katika mapambano dhidi ya udumavu ambao mkoa wa Rukwa unaongoza kitaifa kwa kuwa na udumavu wa asilimia 56.3 na hivyo kuwataka wananchi kushiriki kwa ukamilifu katika maadhimisho hayo yatakayofanyika katika vijiji 339 vya mkoa huo ili kupata elimu stahiki itakayowawezesha kuwaepusha watoto na udumavu.

‘Msingi Mkubwa kabisa wa kupambana na udumavu uko hapa kwenye unyonyeshaji, ni lazima mama anyonyeshe mtoto wake ipasavyo, kina mama huwa wanapuuza wengine kufanya jukumu hili kwasababu labda ya masuala ya kiuchumi lakini pia hata kijamii na kimazoea, sasa hii elimu ndio inapswa kuitoa ndani ya siku hizi saba,kwasababu inakwenda katika vijiji vyote, kinamama wakisikia huu ujumbe pamoja na jamii kwa ujumla na kinababa wote tutaweza kupambana na udumavu,” Alisisitiza.

Aidha amevitaka vyombo vya habari kushiriki katika kufuatilia utekelezaji wa sheria mbalimbali zinazolinda haki za uzazi na ulishaji wa watoto kwa kufanya tafiti, kuandika au kuripoti matukio mbalimbali kama vile utekelezaji wa haki mbalimbali ikiwemo haki ya kupata likizo ya uzazi.

Mh. Wangabo ameyasema hayo alipokuwa akiongea na waandishi wa habari leo tarehe 31.7.2019 katika maandalizi ya maadhimisho ya wiki ya unyonyeshaji ambayo kimkoa itafanyika katika Kijiji cha Kisumbakati, Wilayani Kalambo ambapo maadhimisho hayo yatakwenda sambamba na siku ya Afya ya Kijiji katika vijiji vyote vya mkoa.

Kwa upande wake Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Emanuel Mtika alisisittiza kuwa mradi wa Lishe Endelevu ambao unalenga kupunguza udumavu katika Mkoa wa Rukwa umekuja kuongeza kasi ya juhudi za mkoa katika kupambana na udumavu na kuongeza kuwa maadhimisho hayo yanalenga kujenga uelewa wa pamoja katika unyonyeshaji wa mtoto.

“Siku 1000 za makuzi ya mtoto, ukikosea kwenye eneo la unyonyeshaji kuna uwezekano mkubwa sana wa kumuweka mtoto kwenye mazingira magumu, kwahiyo hii inalenga sit u kutoa elimu ya unyonyeshaji lakini pia juu ya maandalizi ya vyakula vya watoto hawa,” Alisema.

Halikadhalika Kaimu Afisa Lishe wa Mkoa Asha Izina alizitaka sekta binafsi kuwapa muda wafanyakazi kina mama wenye watoto ili aweze kuwanyonyesha watoto wao, “Serikali inatia msisitizo kwamba waajiri wahakikishe nao pia wanatoa nafasi au wanatengeneza mazingira ambayo yanakuwa ni Rafiki pale kazini ambapo mama analetewa kazini mtoto wake na kuhakikisha kwamba anamnyonyesha, tukitambua kwamba maziwa ya mama ni ya muhimu kwa afya na maendeleo ya mtoto”.

Kauli mbiu ya mwaka huu 2019 ni: “Mwezeshe mama aweze kunyonyesha.” Ambayo inasisitiza kuwa kwa pamoja tushirikiane kumwezesha mama aweze kunyonyesha ipasavyo.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa