• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Uvuvi haramu ziwa Tanganyika wakusanya milioni 90 ndani ya mwezi mmoja.

imewekwa Tar: November 14th, 2018

Opresheni ya kupambana na uvuvi haramu katika ziwa Tanganyika kanda ya Kasanga, mkoani Rukwa imefanikiwa kukusanya shilingi milioni 90 ndani ya mwezi mmoja ikiwa ni adhabu mbalimbali kwa wavuvi waliokiuka sheria za uvuvi na.22 ya mwaka 2003 pamoja na sheria ya mazingira na.20 ya mwaka 2004.

Hayo yamesemwa na kiongozi wa operesheni hiyo Geofrey Salaka wakati akitoa taarifa kwa mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo baada ya kutembelea katika soko la samaki la kasanga na kuongea na maafisa wa operesheni hiyo.

Salaka alisema kuwa mbali na kuwatoza faini hizo pia wamefanikiwa kutoa elimu na kuwahamasisha wavuvi wadogowadogo kulipia leseni zao za uvuvi na leseni za vyombo wanavyovitumia kwa shughuli za uvuvi kama sheria inavyotaka huku akielezea changamoto wanazozipata katika kutekeleza majukumu hayo.

“Changamoto tunazozipata ni pamoja na kukumbana na fujo kutoka kwa wananchi utoroshwaji wa samaki na mazao ya uvuvi kwenda nje ya nchi, kuwepo raia wa kigeni wakijihusisha na shughuli za uvuvi, hali ya hewa, upepo mkali, mvua na mawimbi ziwani,” Alisema.

Kwa upande wake Mh. Wangabo alipongeza juhudi hizo za kuhakikisha mapambano dhidi ya uvuvi haramu hayarudi nyuma ili kutunza na kuhifadhi samaki na mazingira katika ukanda wa Ziwa pamoja na Ziwa lenyewe na kusisitiza elimu iendelee kutolewa kwa wavuvi ili washiriki katika kutunza mazingira.

“Tuendelee kuwaelewesha wavuvi, vinginevyo wataendelea kuharibu rasilimali ya taifa letu, na hii ni kwaajili yetu sisi na vizazi vinavyokuja, tukivua katika hali ambayo haina uvuvi endelevu tutawafanya hawa samaki mwishoni watakwisha, wakiisha hawa watu watakwenda wapi, maisha yao yanategemea hapa lakini hawajui hilo, wanataka waharibu mpaka kambi sijui watalala wapi,” Alisema.

Na kuongeza kuwa atahakikisha anafanya mkutano na wananchi na wavuvi hao ili kuweza kuwaelimisha juu ya madhara yanayoweza kujitokeza kama uvuvi haramu utaendelea kutekelezwa bila ya usimamizi wowote.

Operesheni hiyo ilianza tarehe 19.10.2018 na Miongoni mwa zana zilizokamatwa katika operesheni hiyo ni pamoja na Injini za boti 10, mitumbwi 48, magari 9 ya kusafirisha samaki, pikipiki 4 zilizokuwa zinasafirisha samaki, samaki wachanga kilo 2050, nyavu 250 za makila chini ya nchi tatu pamoja na nyavu 20 za timber (monofilament nets).

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa