• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Uzinduzi wa Chanjo ya UVIKO 19

imewekwa Tar: August 4th, 2021

RC MKIRIKITI: "WANA RUKWA JITOKEZENI KUPATA CHANJO YA UVIKO 19 NI SALAMA "

Wananchi wa mkoa wa Rukwa wamehamasishwa kujitokeza kupata chanjo ya kinga dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona ambapo serikali mkoa wa Rukwa imeanza kutoa chanjo kwa wananchi wenye utayari na hiari .

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Joseph Mkirikiti  leo (04.08.2021) amewaongoza wananchi wa mkoa huo kupata chanjo ya kinga dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona ambapo amesema kuwa chanjomhiyo ni salama na inalenga kuwasaidia watu kuwa na kinga imara .

Mkuu huyo amewaeleza wakazi wa Sumbawanga waliokusanyika kwenye hospitali  ya Rufaa ya Mkoa Sumbawanga kuwa serikali ya Awamu  ya Sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imedhibitisha pasipo shaka kuwa chanjo hii ya UVIKO  19 ni salama na kuwa wengi wajitokeze kupata chanjo.

"Rais Samia amesema chanjo hii ni bure na ya hiari kwa mwananchi yeyote mwenye kuhitajinili kujikinga na ugonjwa wa Corona. Mimi leo nitakuwa wa kwanza kuchanja hapa hapa " alisema Mkirikiti

Katika tukio hilo lililohudhuriwa na viongozi wa serikali na dini , wazee maarufu pamoja na wananchi toka wilaya zote za Sumbawanga, Nkasi na Kalambo  wananchi  wengi wamehamasika kupata chanjo hiyo.

Mkirikiti  ameto agizo kwa wakuu wa wikaya kutoa elimu kwa kushirikiana na viongozi wa dini juu ya kudhibiti mikusanyiko na kwenye shughuki za misiba ili kuepuka maambukizi kusambaa.

Mkuu huyo wa mkoa alisisitiza wataalam wa afya kutoa elimu ya kujikinga ikiwemo umuhimu wa kufanya mazoezi hatua itakayosaidia kuongeza kinga ya mwili dhidi ya virusi vya Corona.

Akizungumza kuhusu chanjo hiyo Mganga Mkuuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu  alisema lengo la serikali  kutoa dozi hizo za chanjo ya kinga dhidi ya ugonjwa wa virusi  vya Corona utasaidia kuongeza kinga ya mwili ya mwanadamu .

Aliongeza kusema lengo jingine ni kupunguza gharama za matibabu kwa wagonjwa pia kupunguza idadi ya vifo vinavyotokana na virusi vya Corona.

" Tumepokea dozi za chanjo Elfu Ishirini ambazo tayari zimefikishwa kwenye vituo 11 vilivyoanishwa kutoa chanjo, wananchi naomba tujitokeze kupata chanjo" alisema Dkt. Kasululu

Naye Mzee maarufu wa Sumbawanga Kapteni Mstaafu Nkoswe Noel (81) amefurahi kupata chanjo hiyo na kuiomba serikali kuwafikishia wananchi wengi chanjo ili waepukane na ugonjwa huu hatari wa korona.

Mzee Nkoswe amewasihi wakazi wa Rukwa kujitokeza na kuchanja ili maradhi ya Corona  yasiendelee kuenea nchini  na kuongeza kuwa serikali ilete chanjo zaidi ya 20,000 za sasa.

Kwa upande wake Sheikh wa Mkoa wa Rukwa Rashid Akilimani akizungumza  baada ya kupata chanjo ya UVIKO 19 alisema ameshukuru kupata dozi hiyo kwani itamwezesha mwaka huu kwenda kutekeleza ibada ya Hija.

" Mwaka jana 2020 sikuweza kwenda Hija nchini Saudia baada ya kukosa chanjo ya UVIKO. Leo ninashukuru serikali kutuletea chanjo hii hapa Rukwa" alisema Sheikh Akilimali.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa