• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

VIONGOZI WA TARAFA WAHAMASISHE CHANJO UVIKO-19 RUKWA

imewekwa Tar: October 25th, 2021

RC MKIRIKITI: VIONGOZI WA TARAFA NA VIJIJI WATUMIKE KUHAMASISHA CHANJO YA UVIKO-19

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti ameagiza viongozi wa Tarafa, Kata na Vijiji kuelimishwa na kuhamasishwa ili washiriki kikamilifu kwenye utoaji hamasa ya wananchi kujitokeza kuchanja chanjo ya UVIKO-19 aina ya Sinopharm iliyoanza kutolewa kote mkoani.

Ametoa agizo hilo leo (25.10.2021) mjini Sumbawanga wakati akifungua kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi ngazi ya mkoa kilichokutana kufanya tathmini ya Mpango Harakishi na Jumuishi ya chanjo ya UVIKO-19 awamu ya kwanza.

Mkirikiti alibainisha kuwa changamoto zilizojitokeza kwenye uhamasishaji wa zoezi la chanjo ya UVIKO-19 imeonesha kuwa viongozi wengi ngazi ya chini hawakushiriki kikamilifu kwenye utoaji elimu na hamasa hatua iliyopelekea kuchelewa kukamilika kwa kazi ya uchanjaji kwenye vijiji na mitaa.

“Tuimairishe na kushirikisha watendaji ngazi ya tarafa, kata, vijiji, mitaa na vitongoji ili waweze kutoa elimu na ushawishi kwenye jamii ili watu wengi sasa wapate kuchanja chanjo ya korona aina ya Sinopharm, hatua itakayosaidia kuongeza kinga dhidi ya ugonjwa huo” alisisitiza Mkirikiti.

Akiwasilisha taarifa ya tathmini ya uchanjaji Kaimu Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Alli Lubeba alisema jumla ya wananchi 17,757 walichanja chanjo aina ya J &J ya kinga dhidi ya UVIKO-19 kwenye mkoa wa Rukwa ambapo wanaume waliokuwa 9,575 na wanawake 7,182.

Lubeba alisema pia katika awamu ya pili mkoa wa Rukwa umepokea chanjo ya UVIKO-19 aina ya Sinopharm dozi 24,183 ambapo tayari zimepelekwa kwenye vituo vya kutolea huduma za afya katika halmashauri zote nne.

Ametaja mgao wa chanjo kwa awamu ya pili kwenye kila halmashauri kuwa Kalambo (dozi 3,600), Sumbawanga Manispaa (dozi 4,800), Nkasi (dozi 4,800) na Sumbawanga vijijini (dozi 4,800) aina ya Sinopharm ambapo dozi 6,000 zimesalia kama akiba kwenye famasi kuu ya mkoa.

“Chanjo hii ya aina ya Sinopharm tutaitoa kwa mtu kuchanja dozi mbili ambapo dozi ya pili hutolewa baada ya wiki tatu tangu dozi ya kwanza.Hii ni tofauti na ilivyokuwa dozi za J&J ambapo mtu alipata dozi moja pekee” alisema Lubeba.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya Amani ya Mkoa ambaye pia ni Askofu wa KKKT Dayosisi ya Ziwa Tanganyika Ambele Mwaipopo, alisema ili mafanikio zaidi yapatikane kwenye awamu ya pili ya kuchanja ni budi wataalam wa afya kuyafikia makundi ya jamii kwa karibu ikiwemo makanisani, misikitini, kwenye misiba na matamasha kuwapa elimu ya umuhimu wa chanjo.

Naye Kiongozi wa Machifu Mkoa wa Rukwa Mwene Charles Chilindo Katata wa Himaya ya Nkasi Akizungumza kwenye kikao hicho aliwataka viongozi wa serikali kuwatumia viongozi wa kimila kutoa elimu ya umihimu wa chanjo ya uviko kwani jamii inawaheshimu na kuwasililiza.

Kuhusu uvumi kuwa chanjo ya korona inasababisha kupungua nguvu za kiume Mwene Katata alisema yeye amechanja tayari na hakuna tatizo lolote la kiafya alilopata.

“Sisi wanaume tumechanja na sasa ni miezi mitatu hakuna nguvu iliyopunua.Mambo kwenye familia yapo sawa hivyo si kweli chanjo ya UVIKO -19 inasababisha nguvu za kiume kupungua.” alisisitiza Chifu Katata.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa