• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

WAAGIZWA KUKAMILISHA MAANDALIZI YA CHANJO POLIO

imewekwa Tar: September 15th, 2023

Na Khadija Dalasia  - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa

Tarehe: Septemba 15, 2023

Waganga Wakuu wa Mikoa ya Rukwa, Songwe, Katavi, Mbeya na Kagera wametakiwa kukamilisha maandalizi ya kampeni ya kitaifa ya chanjo dhidi ya Polio inayotarajiwa kufanyika kuanzia tarehe 21 hadi 24 Septemba 2023.

Mganga Mkuu wa Serikali Prof. Tumaini Nagu ametoa maelekezo hayo leo tarehe 15 Septemba 2023 alipofanya kikao na watumishi wa sekta ya Afya Mkoani Rukwa.

Profesa Nagu ametoa maelekezo kwa Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya zilizomo katika Mikoa hiyo kukamilisha maandalizi kabla ya tarehe hizo.

Amesema kuwa Polio ni ugonjwa wa kuambukiza unaosababisha ulemavu wa viungo na unaoweza kusababisha kifo. Njia mojawapo ya maambukizi ni kupitia kinyesi hivyo ametaka wananchi wote wakumbushwe na kuelekezwa kuwa na vyoo bora na kuvitumia kwa usahihi.

Amewataka Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuhakikisha  kila mtoto mwenye umri wa miaka nane kushuka chini anafikiwa pasipo kujali changamoto za kijiografia.

Amewaelekeza kuhakikisha chanjo inapatikana katika maeneo yote yaliyotengwa kwa shughuli hiyo na kuhakikisha hamasa kwa wananchi inatolewa kupitia viongozi wa kidini, watu mashuhuri kijamii na kwa kupitia vyombo vya habari na kurasa za mitandao ya kijamii.

Mkakati maalum umewekwa ili kuhakikisha chanjo hiyo inawafikia watoto wanaoishi katika maeneo ya mbali na maeneo yasiyofikika kwa urahisi kwa kuwa na timu zitakazotoa huduma tembezi.

Profesa Tumaini Nagu ameyashukuru mashirika ya kimataifa, likiwemo Shirika la Afya Duniani (WHO) na UNICEF,  kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa Serikali ya Tanzania katika kutokomeza Polio.

Watoto 391,883 wanatarajiwa kuchanjwa katika Mkoa wa Rukwa.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MIRADI YA BILIONI 56.7 YAKAGULIWA KALAMBO

    September 25, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WAAGIZWA KUKAMILISHA MAANDALIZI YA CHANJO POLIO

    September 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa