• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wafanyakazi Rukwa waaswa kupunguza matumizi ya simu za mikononi muda wa kazi.

imewekwa Tar: May 1st, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaasa wafanyakazi mkoani Rukwa kupunguza matumizi ya simu za mikononi kwaajili ya shughuli binafsi nje na majukumu ya kazi hasa muda wa kazi wanapokuwa ofisini wakiendelea kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Amesema kuwa dhamira ya serikali ya awamu ya tano ni kumtumikia mwananchi kwa nguvu zote hivyo kila mfanyakazi anapaswa kuongeza bidii katika kufanya kazi, lakini kutumia simu na kuacha kuwahudumia wananchi kwa wakati mfanyakazi anakuwa anapata mshahara ambao hausmtahili kutokana na kutotumia muda wake alioajiriwa kwa ufanisi.

“ Ndugu wafanyakazi, hizi simu zimekuwa ni changamoto kubwa sana sehemu zetu za kazi, unakuta mtu badala ya kufanya kazi, hata kutoa huduma kwa mwananchi yeye “ana-chat” kwenye simu, vidole viko kwenye simu, yeye na simu, simu na yeye, kazi haziendi na kama zinakwenda basi zinakwenda kwa mapungufu, kunakuwa hakuna ufanisi na umakini, suala hili la simu tuliangalie sana ndugu waajiri pamoja na waajiriwa,” alisisitiza

Ameongeza kuwa wafanyakazi wamekuwa wakidai maslahi kuliko kupima uwajibikaji wao katika kazi ambazo wanapaswa kuzitekeleza na hali inayopelekea kuzorota kwa kazi nyingi kutokana na wafanyakazi kujishughulisha na matumizi ya simu za mkononi kuliko kuwajibika.

Ameyasema hayo katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani ambayo kimkoa katika mkoa wa Rukwa yalifanyika katika viwanja vya mpira mji mdogo wa Laela, Wilaya ya Sumbawanga alipokuwa akitoa ufafanuzi wa maeneo nane yenye kulenga kuimarisha utendaji wa kazi ili kuleta maslahi kwa wananchi pamoja na wafanyakazi katika maeneo yao ya kazi, ikiwemo uwajibikaji, kushughulikia kero za wananchi, uadilifu, usimamizi wa miradi, ubunifu, ushirikiano,kupambana na Rushwa,na kuunda mabaraza ya kazi.

Wakati akisoma risala ya wafanyakazi kwa mgeni rasmi katibu wa shirikisho la vyama huru vya wafanayakazi (TUCTA) Mkoani Rukwa Nashoni Kabombwe alisema kuwa kuna baadhi ya waajiri hawataki kabisa zoezi la kupata wafanyakazi bora kwenye taasisi zao lifanyike kwa kisingizio kwamba hawana fedha wala zawadi yoyote ya kuwalipa.

Katika kushinikiza hilo alisema, “kiwango cha zawadi kwa wafanyakazi bora zinazotolewa na baadhi ya waajiri ni kidogo na hakiendani na mabadiliko ya kiuchumi TUCTA inawataka waajiri kuanzia sasa kiwango cha chini cha zawadi kiwe shilingi 500,000 au kitu chenye thamani isiyopungua fedha hiyo.”

Kwa upande wake Afisa mfawidhi wa Tume ya Usuluhishi na Uamuzi (CMA) katika mikoa ya Rukwa na Katavi Oscar Ngaluka katika mwaka wa fedha 2017/2018 Tume ilipokea jumla ya migogoro ya kikazi 127, wakati iliyomalizwa katika hatua ya usuluhishi ni 93, na inayoendelea na migogoro ni 10 na kuongeza kuwa sekta inayoongoza kwa migogoro mahala pa kazi katika mikoa ya Rukwa na Katavi ni ujenzi wa barabara.

“Sababu zinazoweza kumfanya mfanyakazi afungue mgogoro wake katika Tume ni pamoja na kuachishwa kazi bila ya kuwepo sababu ya kufaa na utaratibu wala kosa, mwajiri kuzuia vyama vya wafanyakazi kutekeleza majukumu yao ya kichama, madai ya stahili mbalimbali na manyanyazo sehemu za kazi,” Alisema.

Kauli mbiu ya siku ya wafanyakazi ni “Tanzania ya Uchumi inawezekana, wakati wa mishahara na maslahi bora kwa wafanyakazi ni sasa” ambapo Tanzania nzima ina vyama vya wafanyakazi 31 huku Mkoa wa Rukwa ukiwa na vyama vya wafanyakazi 9.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa