• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wajasiliamali wasiotambulika wapewa wiki tatu kujisalimisha

imewekwa Tar: February 1st, 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa wiki tatu kwa wafanyabiashara wadogo wadogo waliopo ndani ya manispaa ya Sumbawanga kuhakikisha wanakuwa na vitambulisho vitakavyowafanya kutambuliwa rasmi na serikali na hivyo kujulikana shughuli zao wanazozifanya katika maeneo mbalimbali ndani ya Manispaa hiyo.

Amesema kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli imedhamiria kuyatambua makundi yote ya wafanyabiashara nchini na katika kufikia lengo hilo imeweka utaratibu maalum wa kuwapatia vitambulisho wajasiliamali ili wasibughudhiwe, na kuongeza kuwa ili waweze kutafutiwa maeneo yao maalum ya kufanyia kazi ni lazima watambuliwe.

“Kama hana kitambulisho hiki ambacho amekitoa Mh. Rais na wakati huo huo hana TIN ya biashara ya TRA sasa yeye ni nani? Narudia kusema kwamba yeyote baada ya wiki tatu ambaye hana kitambulisho, hatauza hata nyanya nje ya mlango wake, kwasababu ni mfanyabiashara mdogo, na kama haupo kwenye ufanyaji biashara mkubwa wa kuwa na TIN na hauna kitambulisho cha ujasiliamali inamaana haufanyi shughuli za biashara,” Alisisita.

Aidha alibainisha makundi ambayo ni walengwa wa vitambulisho hivyo wakiwemo, mafundi baiskeli, wauza mkaa, wauza nyanya, wauza “viosk” mitaani, mafundi seremala wa mitaani, mama ntilie, wauza matunda wa mitaani, waendesha bodaboda, pamoja na wale wote wanaojishughulisha na biashara ambao hawajafikia vigezo vya kusajiliwa na TRA.

Ameyasema hayo katika kikao kazi kilichowakutanisha watendaji wa kata na mitaa wa Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga ili kuzungumzia mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitatu ya serikali ya awamu ya tano katika manispaa hiyo.

Halikadhalika aliwaonya wale wote wanaosita kuchukua vitambulisho hivyo wakidhani kuwa havina umuhimu na kwamba hakuna tofauti ya kuwa nacho na kutokuwa nacho wasubiri baada ya wiki hizo tatu kupita ndipo itajulikana umuhimu wa kitambulisho hicho.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa