• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wajumbe RCC waiomba Serikali kuhuisha Mradi wa VETA Sumbawanga ili kuwakomboa Wananchi.

imewekwa Tar: February 23rd, 2021

Wajumbe wa Kamati ya Ushauri ya Mkoa wa Rukwa (RCC) wameiomba Serikali kukamilisha taratibu za kuendeleza ujenzi wa Chuo cha Ufundi VETA Mjini Sumbawanga ili wanafunzi na makundi mbalimbali ya vijana wanaohitaji kuendelea na ufundi katika Chuo hicho kuweza kunufaika nacho na hatimae kuchochea maendeleo ya Mkoa.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti baada ya kukitembelea na kukikagua chuo hicho kabla ya kuanza kikao cha kamati hiyo inayoongozwa na Mwenyekiti wa kamati ambaye pia ni Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo wamesema kuwa serikali imeshawekeza fedha za kutosha hadi kufikia hatua hiyo baada ya kuachana na mkandarasi aliyeshindwa kumaliza ujenzi huo na hatimae kukiendeleza kwa utaratibu wa “Force Account”.

Mh. Aida Khenan ni Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kaskazini ambaye kwa upande wake alisema kuwa vijana wengi wanaofaidika na asilimia 10 ya mikopo inayotolewa na halmashauri wanashindwa kuendeleza miradi yao kutokana na kutokuwa na elimu ya kutosha kufanya hivyo jambo ambalo lingepunguzwa na uwepo wa chuo hicho mkoani humo.

“Leo tungetemea kwamba ile asilimia 10 inayotolewa na serikali kwaajili ya kukopesha vijana, wanawake na watu wenye ulemavu kumekuwa na changamoto ya marejesho ya ile fedha na sababu ni moja tu, wanapewa fedha na hawana mafunzo ya kitu wanachokwenda kufanya ili waweze kurejesha lakini wale wanaotoka hapa ambao wanakuwa tayari wamepewa amafunzo ya namna ya kujitegemea ingekuwa ni rahisi kuwapa wao waweze kujiajiri na kuwaajiri wenzao,” Alisema.

Nae Mbunge wa Kalambo Mh. Josephat Kandege aliiomba serikali kufanya kila kinachowezekana ili chuo hicho kikamilike na pia kutoa kozi ambazo zingewasaidia wananchi wa mkoa wa Rukwa na maeneo jirani.

“Ukiwa unaanzisha chuo cha VETA ambacho hakijatilia maanani kwamba sisi ni wakulima, matrekta yatakuwepo, tunahitaji vijana ambao watakuwa wamefundishwa waweze kuyatengeneza matrekta badala ya kwenda kufuata mafundi mbali itakuwa tunajidanganya na bahati nzuri wamesema kuwa hiyo wataweka katika kozi ambazo zinatakiwa kuwepo,” Alisema.

Aidha, Mstahiki Meya wa Manispaa ya Sumbawanga Justin Malisawa aliutaka uongozi wa VETA kuhakikisha mazingira ya eneo hilo yanatunzwa baada ya shughuli za ujenzi kusimama tangu tarehe 14.1.2020 huku Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Mh. Daudi Sichone akishauri kamati hiyo kuendelea kufuatilia maendeleo ya chuo hicho ili wananchi wapate walichotaraji.

Wakati akitoa taarifa fupi ya maendeleo ya ujenzi huo msimamizi wa mradi wa ujenzi wa Chuo hicho ch a VETA Jerome Longido alisema kuwa ujezi huo ulitakiwa kumalizika tarehe 22.9.2019 lakini serikali ilimuongezea muda siku 100 mkandarasi Tender International lakini hadi kufikia mwisho wa muda wa nyonyeza tarehe 31.12.2019 mkandarasi huyo alishindwa kukamilisha mradi na hatimae tarehe 14.1.2020 aliandika barua ya kusitisha kuendelea na ujenzi huo ambao mpaka tarehe 23.2.2021 hakuna ujenzi unaoendelea katika eneo hilo.

“Hivi majuzi watu wa Wizara ya Elimu walikuja hapa wakaonesha nia ya kwamba huu mradi ufanyike kwa njia ya ‘force account’ na kuachana na mambo ya mkandarasi, walitoa hayo maelekezo baadaye tukaja na timu ya mkandarasi na mshauri elekezi na sisi VETA tukashirikiana kuona hatua iliyofikiwa ya huu mradi ili kuachana rasmi na mkandarasi, zoezi lilifanyika na makubaliano yamefikiwa, mkandarasi amekubali na sasa kazi imerudi serikalini na sasa mradi utaendeshwa kwa ‘force account’ lakini ni lini utaanza, viongozi wa juu wanajua,” Alisema.

Wakati Mkandarasi anakabidhiwa mradi huo ulikuwa na Gharama za Shilingi Bilioni 10.7 na ujenzi ukikamilika chuo kitaweza kuchukua wanafunzi 900 wa kozi ndefu na 600 wa kozi fupi hivyo, kitakuwa na uwezo wa kuchukua jumla ya wanafunzi 1,500.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa