• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Waliovamia Ziwa Rukwa Waondoshwe

imewekwa Tar: April 11th, 2022

WANANCHI WALIOVAMIA ZIWA RUKWA WAONDOSHWE- RC MKIRIKITI

Na. OMM Rukwa

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti ametoa muda wa siku Thelathini kwa wananchi wanaofanya shughuli za kilimo na makazi ndani ya eneo la mita Sitini kando ya Ziwa Rukwa kuondoka kwa kuwa wanasababisha uharibifu ikiwemo kupungua kwa kina cha ziwa hilo.

Mkirikiti alitoa kauli hilo juzi (08 Aprili 2022) mjini Sumbawanga wakati wa kikao cha wadau wa mazingira kilicholenga kuweka mikakati ya kunusuru uharibifu wa misitu na vyanzo vya maji kote mkoani.

Alisema ni wakati sasa kwa viongozi wa wilaya ya Sumbawanga wakiongozwa na Mkuu wa Wilaya hiyo Sebastian Waryuba kwenda na kuanza kutoa elimu kwa wananchi kupisha maeneo waliyovamia kwenye ukanda wa ziwa Rukwa kwa mujibu wa Sheria.

“Tuhakikishe eneo la mita Sitini kando ya Ziwa Rukwa likiwa bila watu wanaoishi au kufanya shughuli za kilimo na mifugo. Wote waliovamia waondolewe ndani ya siku 30 na nipatiwe taarifa ya utekelezaji .Viongozi nendeni mkasimamie sheria bila kuonea wananchi, “alisisitiza Mkirikiti.

Kwa mujibu wa taarifa ya Mamlaka ya Bonde la Ziwa Rukwa ilisema ziwa hilo lina ukubwa wa mita 88,000 ambapo lina kina cha mita tisa (9) ambazo zinaendelea kushuka kwa kasi kutokana na shughuli za binadamu hivyo tope jingi kujaa.

“Kwa upande wa Ziwa Rukwa kumekuwa na uharibifu mkubwa wa misitu ya Lyamba lya Mfipa hali inayosababisha ziwa Rukwa wakati mwingine kujaa tope. Hivyo wadau wa mazingira mnayo nafasi ya kuhakikisha kuwa mnawaelimisha wananchi kuutunza vyanzo hivi vya maji kwani maji ni uhai” Mkirikiti akihitimisha hotuba yake.

Akizungumza kuhusu uharibifu katika bonde la Ziwa Rukwa, Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Sebastian Waryuba alisema ni kweli Mifugo, kilimo kando ya ziwa hilo pamoja na makazi yanaathiri uhai wa ziwa hilo.

Waryuba aliongeza kusema atatekeleza kazi ya kutoa elimu kwa wananchi wote waliovamia eneo hilo kwa kuwapa elimu juu ya sheria inavyotaka watu wakae umbali wa mita 60 toka ziwani na kuwa kazi hii itafanyika kwa weledi mkubwa.

Kilian Swai ni Afisa Utekelezaji toka Timu ya Mwanasheria Watetezi wa Mazingira kwa Vitendo (LEAT) alisema uharibifu mkubwa wa mazingira unaendelea katika Misitu vya Lyamba lya Mfipa ambako ndio chanzo cha ziwa Rukwa usipodhibitiwa ziwa hilo litatoweka ndani ya miaka 50 ijayo.

Swai aliongeza kusema taasisi yake inafanya kazi na wananchi wa maeneo ya msitu wa Lyamba lya Mfipa kwa kugawa miche ya miti ya matunda na uhifadhi pamoja na kuisaidia kuwekwa kwa mpango wa matumizi bora ya ardhi ili wananchi wasiendelee kuharibu mazingira .

Swai alisema taasisi hiyo imefanikiwa kusambaza miche ya miti 195,000 kati ya lengo la miche 300,000 ili kuhifadhi eneo la msitu wa Lyamba lya Mfipa  ili wananchi watunze mazingira.

Naye Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa ,Kamishna Msaidizi wa Polisi Theopista Mallya alishauri wataalam wa mazingira kutoa elimu kwa wananchi ili watambue kuwa kuvamia maeneo ya vyanzo vya maji na Misitu ni kuvunja sheria kunakosababisha uwepo wa makossa ya jinai.

Kwa mujibu wa Sheria ya Misitu ya namba 14 ya mwaka 2002 inakataza uharibifu wa Misitu unaotokana na ukataji holela wa miti kwenye maeneo yaliyohifadhiwa ikiwemo vyanzo vya maji.

Mwisho.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa