• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi 2,300 Wapata Chanjo ya UVIKO-19

imewekwa Tar: August 18th, 2021

WANANCHI 2,300 WAPATA CHANJO YA UVIKO-19 RUKWA: DKT.KASULULU

Serikali imebainisha mafanikio ya zoezi la kutoa chanjo ya kinga dhidi ya ugonjwa wa virusi vya Corona (UVIKO-19) ambapo wananchi wapatao 2,300 tayari wamejitokeza kupata chanjo hiyo mkoani Rukwa tangu kuzinduliwa kwa zoezi hapo mwanzo mwa mwezi huu.

Hayo yamebainishwa leo (17.08.2021) na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu wakati akiongea na waandishi wa habari kwenye kituo cha Afya Halmashauri ya wilaya Kalambo. 

Mganga Mkuu huyo alisema takwimu zinaonesha tangu kuzinduliwa kwa zoezi la kutoa chanjo hapo Agosti 03 mwaka huu wananchi wengi kwenye wilaya tatu za mkoa wa Rukwa wameendelea kujitokeza ambapo jumla ya watu 2,300 wamekwishapatiwa chanjo kwa hiari kati ya dozi 20,000 zilizopokelewa mkoani.

Dkt. Kasululu akiwa kwenye kituo cha Afya Matai Wilaya ya Kalambo alitumia fursa hiyo kuendelea kuwasihi wananchi kuwa chanjo zinazotolewa na Serikali ni salama na kuwa zimefanyiwa tathmini mathalani hadi sasa kitaifa watu zaidi ya Laki Mbili tayari wamepata chanjo hiyo ya UVIKO 19 kwa mujibu wa takwimu za Wizara ya Afya.

“Kama Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amechanja, Mkuu wa Mkoa wetu Joseph Mkirikiti amechanja nami pia nikiwa Mganga Mkuu wa Mkoa nimechanja pia zaidi ya watu wengi tayari wamechanja hakuna haja ya kuogopa kuchanja chanjo hii ya UVIKO 19” alinukuliwa Dkt. Kasululu.

Alipoulizwa kuhusu changamoto kwenye zoezi hilo Dkt. Kasululu alibainisha kuwa Wilaya ya Kalambo bado kuna mwitikio mdogo ukilinganisha na halmashauri zingine kutokana na baadhi ya taarifa za upotoshaji wa baadhi ya watu.

Awali akifungua kampeni ya usawazishaji wa vikope kwa wananchi wenye matatizo mbali mbali ya macho Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Sebastian Waryoba aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Rukwa aliwasihi wananchi wa Wilaya ya Kalambo kuendelea kujitokeza kupata chanjo ya UVIKO 19 huku wakichukua tahadhari zingine.

Mkuu huyo wa Wilaya alibainisha kuwa pamoja na kuchukua jitihada zingine za kujikinga na UVIKO 19 ni budi wananchi wakaendelea kumwomba Mungu aliepushe Taifa letu na janga la Corona.

“Tuendelee kumwomba Mungu atuepushe na ugonjwa huu wa Corona na Tanzania iendelee kuwa nchi salama huku tukizingatia ushauri wa wataalam wa afya” alisema Waryoba.

Mkoa wa Rukwa ulipokea dozi 20,000 za chanjo UVIKO 19 ambapo awali ilitenga vituo 11 vya kutoa chanjo lakini kutokana na ukubwa na mtawanyiko wa watu imelazimu kuongeza vituo pia kutumia huduma vikoba (mobile clinic) ili kuwafikia wananchi wengi waliopo mbali na vituo vya afya.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa