• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi 57,638 Wapata Chanjo ya UVIKO-19

imewekwa Tar: January 20th, 2022

WANANCHI 57,638 WAPATA CHANJO YA UVIKO-19 RUKWA: DKT. KASULULU

Na OMM Rukwa

Wananchi wa mkoa wa Rukwa wamepongezwa kwa kujitokeza kupata chanjo ya kinga dhidi ya ugonjwa wa Korona ambapo hadi kufikia mwezi Januari mwaka huu watu 57,638 wamefanikiwa kupata chanjo hiyo katika vituo vya afya.

Akizungumza kwenye kikao cha Umoja wa Machifu wa mkoa wa Rukwa jana (19.01.2022) mjini Sumbawanga, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu alisema tangu zoezi hilo la kutoa dozi za chanjo lilipoanza mwezi Julai 2021 kumekuwa   na mwitikio mzuri toka kwa wananchi.

Mganga Mkuu huyo alieleza mafanikio ya chanjo kwa wananchi yaliyopatikana ni pamoja na kupungua kwa watu waliolazwa kwa maambukizi ya korona pia kutokuwepo taarifa za watu waliopata madhara baada ya kupata dozi ya chanjo ya UVIKO-19.

“Kwa kupitia chanjo ya kinga dhidi ya UVIKO-19 hatusikii tena kusongamana kwa wagonjwa wodini hata vifo vimepungua kwenye mkoa wetu. Rukwa tulipokea dozi 68,683 za chanjo ya UVIKO-19 ambapo watu 57,638 sawa na asilimia 84 tayari wamechanjwa” alieleza Dkt. Kasululu.

Kwa upande wake Chifu Kiongozi wa Machifu Mkoa wa Rukwa na Mkuu wa Mkoa Mstaafu Joachim Wangabo aliwasihi Machifu kwenda kuelimisha na kuhamasisha jamii hususan Wazee kujitokeza kupata chanjo.

Chifu Wangabo alisema yeye binafsi tayari amechanja na kuwa leo pia atarudia kupata dozi ya pili ya chanjo ili kukamilisha kwa mujibu wa utaratibu wa wataalam na kuongeza kuwa serikali imelenga kuwafanya wananchi wake wawe salama na wenye kinga dhidi ya ugonjwa wa UVIKO-19.

Akizungumza kwenye kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti aliwataka viongozi hao wa Machifu kufundisha maadili mema kwa jamii ili amani na maendeleo kwa mkoa yaendelee kupatikana kwani viongozi hao wanaheshimika vizuri kwenye jamii.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa