• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

WANANCHI RUKWA WATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI DHIDI MPOX

imewekwa Tar: August 14th, 2024



Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kupitia Idara ya Afya imeanzisha kampeni ya kuelimisha umma kuhusu ugonjwa wa MPOX (Monkeypox). MPOX ni ugonjwa unaoambukizwa kutoka kwa wanyama kwenda kwa binadamu na pia kati ya binadamu wenyewe kwa wenyewe.


Akizungumza katika kikao cha maandalizi ya mapokezi ya Mwenge wa Uhuru Mkoani Rukwa leo, Agosti 14, 2024, Mganga Mkuu wa Mkoa, Dkt. Ibrahim Isack, ameeleza kuwa kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), dalili za MPOX ni pamoja na homa kali, vipele, na maambukizi katika ngozi.


Dkt. Isack ameeleza kuwa kuwa ugonjwa huo unaweza kuenea kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kupitia kugusana moja kwa moja na ngozi ya mtu aliyeambukizwa, kujamiiana, kubusiana, au kukaa na mtu aliyeambukizwa katika eneo lisilo na mzungumko mzuri wa hewa, na majimaji kutoka kwa mtu aliyeambukizwa.


Mganga Mkuu wa Mkoa ameongeza kuwa inamchukua mgonjwa kati ya siku 5 hadi 21 kuanza kuonesha dalili za maambukizi. Katika kipindi hicho chote, virusi huwa kwenye damu, na baada ya muda, dalili kama vile homa, maumivu ya kichwa, uchovu, na vipele huanza kujitokeza.


Amesema ugonjwa huo unaweza kusababisha athari kama vile upofu, uvimbe wa njia ya hewa, nimonia, sepsisi, kuharibika kwa mimba, na hata kifo. Aidha, ugonjwa huo unaweza kuharibu ngozi, kusababisha upotevu wa rangi ya ngozi.


Dkt Isack ameeleza kuwa watoto, watu wenye upungufu wa kinga mwilini, wako katika hatari zaidi ya kupata ugonjwa huo.


Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kupitia Idara ya Afya, inawahimiza wananchi kujiepusha na mazingira yote yanayoweza kusababisha maambukizi huku ikielezwa kuwa njia za kujikinga ni pamoja na matumizi sahihi ya barakoa na glovu wakati wa kuhudumia wagonjwa na kuepuka kugusana na wanyama pori hasa wale ambao ni wagonjwa au waliokufa.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa