• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

"Wananchi tujitolee Damu" Dk. Kigwangala

imewekwa Tar: July 22nd, 2017

Naibu Waziri wa Wizara ya Afya Dk. Hamis Kigwangala amesikishwa na hali ya hospitali ya mkoa wa Rukwa kukosa damu ya kutosha kusaidia wagonjwa pindi dharura inapotokea.

Masikitiko hayo aliyatoa baada ya kufanya ukaguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa katika ziara yake ya siku moja ambapo alitembelea hospitali hiyo pamoja na vituo vya afya vitatu vya Laela Wilayani Sumbawanga, Wampembe na Nkomolo vya Wilaya ya Nkasi.

“Nimesikitishwa na changamoto ya upatikanaji wa damu, kwanza mna units chache mlipaswa kuwa na units karibu 120 ili kuendana na idadi ya watu milioni 1.2 wa mkoa mzima, lakini kwa bahati mbaya hamna hata damu moja ambayo imekuwa “screened” na tayari kwa matumizi, hii inasikitisha sana lakini kwa ujumla maabara iliyopo ni nzuri sana, kuna mapungufu machache sana kwenye “theatre” na pia nimefurahishwa na “labour ward” iko vizuri sana.

Dk. Kigwangala alibainisha kuwa changamoto ya upatikanaji wa damu ipo katika kanda ya nyanda za juu kusini na kuahidi kulishughulikia jambo hilo huku akiwaasa wananchi kuweza kujitokeza kwa wingi kuchangia damu na si kukaa vipembeni na kulalamika pindi wanapokosa damu hospitali wakati wanashindwa kujitolea damu.

“Mimi binafsi najitolea damu mara tatu kwa mwaka, wananchi tunatakiwa kujitolea damu ili kuweza kuwasaidia wale wanaohitaji, huwezi jua inaweza kumsaidia ndugu, jirani ama rafiki, hivyo tuwe na moyo wa kujitolea.” Alisema.

Katika ziara yake hiyo mambo aliyoyapa kipaumbele ni kuangalia huduma za maabara, vyumba vya upasuaji, vyumba vya kuzalia pamoja na akiba ya damu salama, ambapo vituo hivyo vilionekana kufanya vizuri katika maeneo hayo.

Huduma ya maji katika vituo hivyo ilioneka kuwa ni kikwazo katika upatikanaji wa huduma bora hivyo Dk. Kigwangala aliwaagiza wakurugenzi wa Sumbwanga Vijijini pamoja na Halmashauri ya Nkasi kuhakikisha jambo hilo linatafutiwa ufumbuzi wa haraka kwa kutambua umuhimu wa maji na ubora wa huduma za afya.

Dk. Kigwangala hakutaka ziara hiyo iwe ya kiutendaji pekee hivyo alikutana na wananchi wa maeneo ya Laela pamoja naWampembe na kuwapa nafasi ya kueleza vikwazo wanavyokutana navyo katika kupata huduma bora ya afya.

Ndipo alipojitokeza ndugu Nassoro Ibrahim na kutaka kufahamu nafasi ya walemavu katika kupata huduma bure kama ilivyo katika makundi ya wazee, watoto na wajawazito, “Naomba Serikali ituangalie na sisi walemavu tunnapata shida sana maana wenzetu wazee, watoto na kinamama wanasaidiwa,”Alisema.

Katika kujibu swali hilo Dk. Kigwangala alimtaka mlemavu huyo kuonana na uongozi ili aweze kufuata taratibu za kuweza kutibiwa bure lakini alimuahidi kuwa serikali ipo katika mkakati kuona namna ambayo wanaweza kuwasaidia walemavu katika kupata huduma bure.











Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MIRADI YA BILIONI 56.7 YAKAGULIWA KALAMBO

    September 25, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WAAGIZWA KUKAMILISHA MAANDALIZI YA CHANJO POLIO

    September 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa