• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi wahimizwa kuanza ujenzi wa Zahanati na Vituo vya Afya kabla ya Serikali kusaidia.

imewekwa Tar: January 20th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga kufuatilia na  kusimamia wananchi wa vijiji 12 vya bonde la ziwa Rukwa kuhakikisha kuwa wanaanza kujenga zahanati ili zahanati hizo ziweze kupunguza mzigo kwa vituo vya afya na hospitali ya wilaya.

Amesema kuwa ili hospitali ya Wilaya isiweze kuzidiwa na wagonjwa ni vyema vijiji vikawa na zahanati zao na kwa ngazi ya kata kuanza ujenzi wa vituo vya afya ili mgonjwa apitie katika ngazi hizo na hatimaye kufika katika ngazi ya hospitali ya wilaya tofauti na hapo hospitali hiyo inaweza kutumiwa na hata wagonjwa ambao wanaweza kutibiwa katika ngazi ya zahanati.

“Kwa upande wa vituo vya afya, jamani nisikitike hapa, katika kata 13 ambapo kila kata inapaswa iwe na kituo chake cha afya tunavyo vituo vya afya viwili peke yake, tuna kituo cha afya pale milepa na kituo cha afya hapa mtowisa, kwahiyo kata 11 hazina vituo vyake vya afya, kwahiyo hapa pia DC jipange tuanze,” Alisema.

Mh. Wangabo aliyasema hayo wikiendi hii katika songambele ya kuchimba msingi wa majengo saba kwaajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya katika kata ya Mtowisa na kuhusisha wananchi kutoka katika vijiji 10 na madiwani 13 wa kata zote za bonde la ziwa Rukwa ambapo hospitali hiyo inajengwa.

Akitoa taarifa ya ujenzi wa hospitali hiyo, mganga mkuu wa halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Fani Musa alisema kuwa hospitali hiyo itatumika kama kituo cha rufaa kutoka vituo vya afya na zahanati zote za halmashauri ya wilaya ya Sumbawanga na kuongeza kuwa mradi utagharimu shilingi Bilioni 7.5 hadi kumamilika kwake ambapo itakuwa na majengo 22 na mpaka sasa halmashauri imepokea shilingi bilioni 1.5 kwaajili ya kuanza ujenzi huo.

“Fedha hizi za awamu ya kwanza zitatumika kujenga majengo saba, jengo la Utawala ambalo litatumia shilingi milioni 332, jengo la wagonjwa wa nje litatumia shilingi milioni 271, jengo la “Pharmacy” litatumia shilingi milioni 120, jengo la maabara litatumia shilingi milioni 171, jengo la vipimo vya mionzi (radiology, X-ray na Ultra Sound) litatumia shilingi milioni 121, jengo la kufulia litatumia shilingi milioni 110 na jengo la mwisho ni la wazazi litakalotumia shilingi milioni 379,” Alisema.

Katika hatua nyingine Mh. Wangabo amewataka wakala wa umeme vijijini kuhakikisha wanaongeza kasi ya kufikisha umeme kwenye bonde hilo ambalo lina wakulima wengi wa mahindi na mpunga pamoja na wavuvi ambapo mazao yao mengi huvushwa na kupelekwa mikoa ya jirani hivyo kuukosesha mkoa mapato na pia kwaajili ya kusaidia huduma za kiafya katika bonde hilo na kuongeza kuwa bila ya halmashauri kuongeza kasi ya kukusanya mapato malengo hayo ya kumalizia maboma hayatafikiwa.

Bonde la ziwa Rukwa lina vijiji 63, kati ya vijiji hivyo vijiji 24 vina zahanati, vijiji 17 vina maboma ya zahanati ambayo hayajaezekwa na vijiji 12 havina zahanati wala maboma, na kati ya kata 13 zilizopo katika bonde hilo ni kata 2 tu ndio zenye vituo vya afya na kufanya kata 11 kukosa vituo vya afya huku kata 3 zikiwa na maboma ya vituo hivyo.

 

 

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa