• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi wakumbushwa kulinda vyanzo vya maji wakati Kata 3 zikinufaika na mradi

imewekwa Tar: September 15th, 2020

Wananchi wa Kijiji cha Kalumbaleza na vitongoji vyake katika bonde la ziwa Rukwa, Wilayani Sumbawanga, Mkoani Rukwa wamehimizwa kuendelea kulinda na kutunza vyanzo vya maji vinavyowasaidia kuendelea kupata maji katika kipindi chote cha mwaka ili kuepukana na shida ya kutafuta maji katika umbali mrefu wakati wakisubiri kukamilika kwa mradi wa maji wa MUZE GROUP unaotarajiwa kumalizika mwezi Novemba mwaka huu

Hayo yamesisitizwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alipokutana na wananchi baada ya kutembelea mradi huo wa maji utakaohudumia vijiji 10 vya kata 3 za Muze, Mwadui na Kalumbaleza na kuwataka wananchi hao kutolima na kufanya shughuli za kibinaadamu karibu na vyanzo hivyo pamoja na kuilinda miundombinu ya maji inayoendelea kusimikwa katika maeneo mbalimbali ya vijiji hivyo.

Aidha, Mh. Wangabo ametoa tahadhari kwa vijiji vya wilaya ya Nkasi vilivyopo juu ya milima ya Lyamba lyamfipa wanaoendelea kufanya shughuli za kibinaadamu kuacha kufanya hivyo kwani uhai wa Maisha ya watu wa bonde la ziwa rukwa unategemea utunzaji wa mazingira wa wananchi wanaoishi kanda ya juu ya safu za milima hiyo.

“Halafu wale ambao wapo wilaya ya Nkasi vile vijiji viwili, nitawafuata huko huko ili watunze mazingira ninyi huku mpate maji ya uhakika, vinginevyo hii kazi itakuwa kazi bure, kama wale wasipotunza mazingira wanakata miti hovyo kwenye chanzo cha maji ninyi huku hamtapata maji, kuna vijiji viwili vya Nkasi, nitavifuata huko huko juu, lakini ninyi cha hapa chini mtimize wajibu wenu, chini ya mwenyekiti wenu serikali ya Kijiji,” Alisisitiza.

Kwa upande Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Wilaya ya Sumbawanga Mhandisi Gibon Nzowa alisema kuwa mradi huo unalenga kuweka vituo 65 pamoja na matenki matano katika vijiji hivyo 10 huku wakitegemea kulaza bomba za kusambazia maji kwa Zaidi ya km 60 na kisha kueleza changamoto zinazokwamisha zoezi hilo.

“Changamoto tuliyokutana nayo mheshimiwa mkuu wa mkoa ni mvua nyingi kipindi cha masika tulikwama kidogo, vile vile changamoto nyingine ni uchafuzi wa chanzo juu katika vijiji vilivyopo wilaya ya Nkasi na kuchelewa kupata fedha kwa wakati,” Alisema.

Mmoja wa wanakitongiji cha katoro katika Kijiji cha Kalumbaleza Emanuel Michael aliiomba serikali kuona uwezekano wa kuwekewa bomba katika kjiji chao ambacho kipo karibu na Kijiji cha Kalumbaleza na kusema “nafikiri wale waliokuja kupima huu mradi, walifika wakapima kule katoro, kule tunakunywa maji ya visima lakini cha ajabu kule hakuna bomba hata moja lakini sisi ni wakazi wa Kijiji cha Kalumbaleza na kata ya kalumbaleza.”

Katika hatua nyingine Mh. Wangabo ameipongeza Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira Wilaya ya Sumbawanga pamojana Mkurugenzi wake kwa kutoa ajira Zaidi ya 300 katika utekelezaji wa mradi huo huku wakiokoa zaidi ya Bilioni 3 kwa kutarajiwa kuukamilisha mradi huo kwa bilioni 3.1 balaya ya bilioni 6 za awali huku fedha hizo zikitolewa na serikali kwa asilimia 100. Vijiji vitakavyofaidika na mradi huo ni Kalumbaleza A na B, Muze, Mnazi mmoja, Mnazi Asilia, Ilanga, Isangwa, Mbwilo, Uzia na Kalakala. 

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa