• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi wapongeza Juhudi za Serikali kupambana na wavuvi haramu ziwa Rukwa.

imewekwa Tar: May 19th, 2017

Wananchi wa bonde la ziwa Rukwa wamepongeza serikali ya Mkoa wa Rukwa kwa juhudi za kuhakikisha mazalia ya samaki katika ziwa Rukwa yanaendelea kuwa salama kwa kupambana na wavuvi haramu wanaoharibu mazingira ya ziwa hilo.

Pongezi hilo zilijitokeza wakati wa ziara ya kamati ya ulinzi na usalama iliyokwenda kuangalia usalama wa ziwa hilo na kufanikiwa kukamata nyavu haramu 188 zenye thamani ya wastani wa shilingi milioni 78 na kuzichoma mbele ya wananchi wanaoishi kwenye kambi ya wavuvi katika kijiji cha Ilanga, Kata ya Mfinga ili kuonesha mfano kwa wale wanaoendelea kutumia nyavu hizo kuharibu mazingira.

Zoezi hilo la kuchoma moto nyavu hizo haramu liliongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen akiwa na Katibu Tawala wa Mkoa, Tixon Nzunda, Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Halfan Haule pamoja na kamati za ulinzi na usalama ya Mkoa na Wilaya.

Katika kuhakikisha kuwa ziwa hilo linaendelea kutunzwa na kulindwa Mh. Zelote aliomba ushirikiano wa wananchi kuhakikisha wavuvi haramu wanafichuliwa na kuchukuliwa hatua zinazostahiki ili iwe fundisho kwa wale wanaoendelea kufanya shughuli hizo bila ya kufuata taratibu na sheria.

“Hili ziwa ni lenu, Mkuu wa Mkoa wala Katibu Tawala hawaji kuvua samaki hapa, ni nyinyi, hivyo ni vizuri mkawa walinzi wa kwanza kabla serikali haijatumia nguvu nyingi kulinda eneo hili, Kila mmoja awe Mlinzi wa mwenzake na kila atakayetoa taarifa tutamlinda kwa sheria zilizopo,” Mkuu wa Mkoa alieleza.

Katika kusisitiza ulinzi huo Mh. Zelote alitoa agizo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kurudisha asilimia 20 ya mapato yanayopatikana kutokana na uvuvi ili kuleta maendeleo kwa wananchi.

Mmoja wa wananchi Paulo Mwang’onda alijitokeza kuipongeza serikali ya Mkoa wa Rukwa kwa juhudi zake za kuhakikisha wavuvi haramu wanakosa nafasi ya kuendelea kumaliza mazalia ya samaki.

“Naiunga mkono Serikali kuutokomeza uvuvi haramu, kwasababu wanaharibu mazalia ya samaki ambao ni faida kwa vizazi vyetu vijavyo, na naiomba serikali itupe ushirikiano pale tunapotoa taarifa za uvuvi haramu,” Paulo alisema.

Sambamba na hilo Mh. Zelote hakusita kuwakumbusha wananchi kuwa makini na ugonjwa hatari wa Ebola mbao upo katika nchi ya jirani y aJamhuri ya Watu wa Kongo (DRC) na kueleza kuwa ugonjwa huo hauna tiba na kuwaeleza dalili za ugonjwa huo.

“Dalili ni homa kali, kutapika, kulegea, kutokwa damu ndani na nje ya mwili na ikitokea umeumwa kimbilia zahanati, kwa daktari, usiseme nanunua Panadol, serikali ya Tanzania haitaki kuwapoteza watu wake.” Mh. Zelote Alifafanua.

Na katik kuhakikisha wananchi hao wanaondokana na udumavu, Mh. Zelote aliwasisitiza wananchi hao kuwa na utaratibu wa kuhifadhi chakula cha kutosha na kuacha kuuza mazao yote wanayovuna kwa lengo la kupata pesa huku wakiwa hawana chakula.  

Katika kuhakikisha ulinzi na usalama unaimarishwa katika bonde la ziwa Rukwa Mkuu wa Mkoa aliahidi kutoa mifuko ya “Cement” 150 ili kumalizia ujenzi wa vituo viwili vya polisi, mifuko 100 kwa kituo cha polisi cha Mtowisa na mifuko 50 kwa kituo cha polisi cha Ilemba.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa