• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi wasisitizwa kuitumia wiki ya sheria kama fursa ya mafunzo ya bure ya sheria.

imewekwa Tar: January 24th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi mkoani humo kuhakikisha wanafika katika mabanda ya kutolea elimu ya sheria ili kuitumia fursa ya kupata elimu hiyo inayotolewa bure kwa kipindi cha wiki nzima ya sheria.  

Mh. Wangabo amesema kuwa elimu hiyo inayotolewa na Mahakama Pamoja na wadau wengine ikiwemo Mawakili wa Kujitegemea, Serikali, Jeshi la Polisi, Ofisi ya Mkurugenzi wa uendeshaji wa Mashataka (DPP), Ofisi ya Wakili (Solicitor General), Baraza la Ardhi Pamoja na Taasisi mbalimbali itawawezesha wananchi hao kuona njia za kutatua migogoro mbalimbali.

Amesema kuwa wananchi wamekuwa na malalamiko na migogoro mingi inayohusu mambo ya kisheria na hawajui sheria na hivyo kuwataka kuitumia wiki hiyo ya sheria iliyoanza tarehe 23.1.2021 kupata ushauri katika changamoto mbalimbali za kisheria wanazokabiliana nazo katika kutafuta haki zao.

“Elimu ni ya Bure itumieni hapa, kwa wale ambao watashindwa kufika hapa, wasikilize vyombo vya Habari, wasome magazeti, wafuatilie kule, kuna elimu ya bure ambayo inatolewa wiki nzima hii, tusikilize redio, watumishi wa mahakama wamejipanga, mahakimu majaji wanatoa elimu kule ya bure na wakati mwingine kutakuwa na mawasiliano ya moja kwa moja, unauliza swali lako utajibiwa.”

“Naona watu wengi sana wanamsumbua Mkuu wa Wilaya wakifikiri yeye ndio hakimu yeye ndio Jaji, yeye ndio mwanasheria, mtu anadhani akienda kule migogoro yake yote inaishia kule, sikilizeni fuatilieni vyombo vya Habari, ili muweze kujua masuala ya kisheria, si kila jambo linatatuliwa na mkuu wa Wilaya, Mkuu wa mkoa, Sisi tunafanya upatanishi ili watu waridhiane tu basi, lakini ukitaka haki ni mahakamani,” Alimalizia.

Mh. Wangabo ameyasema hayo wakati akifungua wiki ya sheria nchini leo tarehe 24.1.2021 kwa Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Sumbawanga, wiki ambayo imeambatana na matukio ya kutembea umbali wa kilomita 9 pamoja na maadhimisho ya miaka 100 tangu kuanzishwa kwa Mahakama Kuu nchini.

Aidha, Mh. Wangabo ametumia nafasi hiyo kuipongeza Mahaka kuu ya Tanzania kwa kuadhimisha miaka 100 (karne moja) tangu kuanzishwa kwake mwaka 1921 huku akiwashauri kutafakari kwa kina mambo yanayotakiwa kuboreshwa ili kuendelea kudumisha Amani, Uhuru, Udugu na Haki kwaajili ya ustawi wa nchi yetu.

Wiki hii ya Sheria inaongozwa na kauli mbiu ya miaka 100 ya Mahakama kuu nchini isemayo; “Mchango wa Mahakama katika nchi inayozingatia Uhuru, Haki, Udugu, Amani na Ustawi wa Wananchi 1921 – 2021”.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa