• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi watakiwa kuacha kulalamika na badala yake waisaidie serikali ili kuijenga nchi.

imewekwa Tar: March 7th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi kuacha kutoa lawama kwa serikali kila uharibifu wa miundombuinu unapotokea na kudai kurekebishiwa na badala yake kuwataka kuwa walinzi kwa wale wanaoharibu miundombinu hiyo ili kuisadia serikali kuokoa fedha nyingi katika kurekebisha miundombinu hiyo na hatimae kuzielekeza fedha hizo katika maeneo mengine muhimu.

Mh. Wangabo amesema kuwa kila kukicha shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji Pamoja na kuharibu miundombinu zimekuwa zikipigiwa kelele lakini wananchi wamekuwa wakiziba masikio na kuwafumbia macho wale wanaoihujumu miundombinu hiyo na kuwa mstari wa mbele kuinyooshea kidole serikali kanakwamba wao sio sehemu ya serikali hiyo.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika mkutano na wananchi wa Kijiji cha Kaoze, kata ya Kaoze, Bonde la Ziwa Rukwa, Wilauyani Sumbawanga baada ya wananchi hao kulalamikia ubovu wa barabara hali inayowafanya wananchi hao kushindwa kutoka wala kuingia ndani ya vijiji vyao pale mvua zinapozidi na hatimae mito kujaa na madaraja kusombwa.

“Pamoja na umuhimu wa barabara hiyo nataka mnipe ufumbuzi wa pale (Kijiji cha) Chombe ambapo huwezi kupita pale, tunafanya nini, ukitaka kuwahamisha wale watasema nilipe, nani anawalipa, mtawalipa ninyi wananchi mnaotaka hiyo barabara, tukitaka kupaunganisha pale mchange fedha zenu muwalipe wale halafu muwatoe, halafu hawa TANROAD na TARURA ‘wa-survey’ tuone tunapitisha wapi hiyo barabara,”

“Kwasababu kuna korongo kubwa kwelikweli pale, yaani huwezi kupita pale, tulipita kwabahati bahati pembeni karibu na shamba, halafu tukakutana na ng’ombe na hatukwenda tena mbele, haya ndio yanayotokea huku kwetu, sasa nataka wananchi mnaponipa mimi ombi kama hilo na ninyi mniambie tunafanye pale chombe, mtakaa kwenye WardDC yenu, Diwani we ni Mwenyekiti wa kAmati ya Maendeleo ya Kata, mzungumzie suala hili la uharibifu wa barabara hasa, kulima kwenye vyanzo vya maji lakini pili mifugo, ng’ombe wanatembezwa barabarani wanaharibu barabara,” Alisisitiza.

Aidha, Amesema kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua wale wote wanaokiuka sheria na kuwa ipo mbioni kuikabidhi safu ya milima ya Lyamba Lyamfipa Kwa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) baada ya watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kuonekana kushindwa kudhibiti wananchi wanaoharibu mazingira ya safu hizo na hivyo kuendelea kuwaasa wananchi kuacha kuharibu maizingira na vyanzo vya maji kutoka katika milima hiyo.

 

 

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa