• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi watakiwa kuacha kulalamika na badala yake waisaidie serikali ili kuijenga nchi.

imewekwa Tar: March 7th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi kuacha kutoa lawama kwa serikali kila uharibifu wa miundombuinu unapotokea na kudai kurekebishiwa na badala yake kuwataka kuwa walinzi kwa wale wanaoharibu miundombinu hiyo ili kuisadia serikali kuokoa fedha nyingi katika kurekebisha miundombinu hiyo na hatimae kuzielekeza fedha hizo katika maeneo mengine muhimu.

Mh. Wangabo amesema kuwa kila kukicha shughuli za kibinadamu katika vyanzo vya maji Pamoja na kuharibu miundombinu zimekuwa zikipigiwa kelele lakini wananchi wamekuwa wakiziba masikio na kuwafumbia macho wale wanaoihujumu miundombinu hiyo na kuwa mstari wa mbele kuinyooshea kidole serikali kanakwamba wao sio sehemu ya serikali hiyo.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika mkutano na wananchi wa Kijiji cha Kaoze, kata ya Kaoze, Bonde la Ziwa Rukwa, Wilauyani Sumbawanga baada ya wananchi hao kulalamikia ubovu wa barabara hali inayowafanya wananchi hao kushindwa kutoka wala kuingia ndani ya vijiji vyao pale mvua zinapozidi na hatimae mito kujaa na madaraja kusombwa.

“Pamoja na umuhimu wa barabara hiyo nataka mnipe ufumbuzi wa pale (Kijiji cha) Chombe ambapo huwezi kupita pale, tunafanya nini, ukitaka kuwahamisha wale watasema nilipe, nani anawalipa, mtawalipa ninyi wananchi mnaotaka hiyo barabara, tukitaka kupaunganisha pale mchange fedha zenu muwalipe wale halafu muwatoe, halafu hawa TANROAD na TARURA ‘wa-survey’ tuone tunapitisha wapi hiyo barabara,”

“Kwasababu kuna korongo kubwa kwelikweli pale, yaani huwezi kupita pale, tulipita kwabahati bahati pembeni karibu na shamba, halafu tukakutana na ng’ombe na hatukwenda tena mbele, haya ndio yanayotokea huku kwetu, sasa nataka wananchi mnaponipa mimi ombi kama hilo na ninyi mniambie tunafanye pale chombe, mtakaa kwenye WardDC yenu, Diwani we ni Mwenyekiti wa kAmati ya Maendeleo ya Kata, mzungumzie suala hili la uharibifu wa barabara hasa, kulima kwenye vyanzo vya maji lakini pili mifugo, ng’ombe wanatembezwa barabarani wanaharibu barabara,” Alisisitiza.

Aidha, Amesema kuwa Serikali haitasita kuwachukulia hatua wale wote wanaokiuka sheria na kuwa ipo mbioni kuikabidhi safu ya milima ya Lyamba Lyamfipa Kwa Wakala wa Misitu Tanzania (TFS) baada ya watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kuonekana kushindwa kudhibiti wananchi wanaoharibu mazingira ya safu hizo na hivyo kuendelea kuwaasa wananchi kuacha kuharibu maizingira na vyanzo vya maji kutoka katika milima hiyo.

 

 

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa