• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi wazuia msafara wa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa wakidai shule

imewekwa Tar: November 14th, 2018

Wananchi wa kitongoji cha Senje, kijiji cha Samazi Wilayani Kalambo wamefanikiwa kuuzui msafara wa mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo na kumuomba kuwawezesha wapate ushirikiano wa kujenga shule ili watoto wao waweze kusoma.

Wananchi hao wameeleza kuwa shule ya msingi iliyopo karibu ni kilomita saba kutoka katika kitongoji hicho ambapo shule hiyo ipo katika kijiji cha Samazi huku watoto hao wengi wadogo wakishindwa kufika katika shule hiyo kutokana na umbali.

Kitongoji hicho cha Senje ambacho ni kipya kimeanza kukaliwa na wananchi na kuonesha maendeleo baada ya kuanza kujenga vyumba viwili vya madarasa, kuchimba shimo la choo pamoja na kuwa na mabati kwaajili ya kuezeka majengo hayo huku wakiwa na suluhisho la dharura kwa kumlipa posho mwanafunzi aliyemaliza kidato cha nne ili aweze kuwafundisha watoto wao.

Kwa upande wake Mh. Wangabo alisema kuwa shule hiyo inayojengwa katika kitongoji hicho itaanza kuwa shule shikizi ya shule ya msingi samazi hivyo watoto hao wataanza kusoma shule ya awali, darasa la kwanza hadi la tatu kasha watahamia katika shule ya msingi samazi wakati taratibu nyingine zikiendelea.

Aliongeza kuwa ili vyuma hivyo vianze kutumika ni muhimu kuwa na ofisi ya mwalimu na nyumba ya mwalimu ili halmashauri iweze kuunga mkono kwa kumleta mwaalimu na watoto waanze kusoma na kuwashauri kuongeza kasi ya ujenzi wa majengo hayo ili waweze kupewa mwaalimu haraka iwezekanvyo kwakuwa serikali ya wamu ya tano isingependa kuwaona watoto hawaendi shule.

“Kata pamoja na kijiji watasimamia hii, mkurugenzi utafuatilia kuhakikisha kwamba mtendaji wa kijiji na kata watasimamia ujenzi ule unaoendelea pale, lazima nyumba ya mwalimu isimame na ofisi ya mwali isimame na wakati huo muendelee kujipanga kuna swala la madawati watoto wasije wakakaa chini, vyoo ni uhimu ili wanafunzi watumie vyoo sio kwenda kwenye vichaka, shule haiwezi kuanza bila ya vyoo, tutaneza milipuko,” Alisisitiza.

Katika kuhakikisha jambo hilo linafanikiwa Mkuu wa mkoa alimuagiza mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya kalambo kuhakikisha wanaunga mkono kwa kununua mbao za kupaulia huku ofisi yake ikichangia bati za ofisi ya mwalimu pindi itakapokamilika.

Katika msafara huo ambao aliwepo mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Julieth Binyura nae aliwataka kuhakikisha ujenzi wa shule hiyo hauishii kwenye madarasa mawili tu na hatimae kuiachia serikali mzigo wa kuendelea kujenga shule hiyo wakati kitongoji hicho hakikuwahi kuwepo.

“Serikali sasa hivi ina utaratibu wa kusajili, kama hujatimiza vigezo huwezi kusajiliwa shule, hata mkiwa mmejenga vyumba viwili lazima mujenge ili mtoto akimaliza la kwanza, la pili, la tatu anaendelea, lakini wengine wakijenga vyumab wanaishia viwili tu halafu watoto wanaanza kusomea chini ya miti hatutaki,” Alibainisha.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa