• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wanarukwa wahamasishwa kulima kwa tija ili kujiongezea kipato

imewekwa Tar: December 2nd, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wakulima wa Mkoa huo kuhakikisha wanafuata maelekezo ya maafisa kilimo waliopo kwenye ngazi za vijiji na kata ili kuweza kulima kwa tija na hatimae kuongeza upatikanaji wa chakula katika mkoa na pia kujiongezea kipato.

Amesema kuwa ni dhamira ya mkoa kuhamasisha kilimo kinachoongeza uzalishaji kwa ekari moja, hivyo ni lazima wakulima wapande kwa kutumia utaalamu huku wakizingatia ubora wa mbegu ambazo zimehakikiwa na Taasisi ya Kudhibiti Ubora wa Mbegu nchini (TOSC) pamoja na kutumia mbolea zinazostahili kwa ekari kama ambavyo wataalamu wanashauri

“Sio mtu anachukua mfuko mmoja wa mbolea halafu anakwenda kuuweka katika ekari mbili matokeo yake uzalishaji  unakuwa ni mdogo, lakini pia baada ya mahindi kuwa yameota na kuwekewa mbolea ni lazima pia kuangalia upande wa visumbufu, wadudu wale waharibifu wa mazao, lazima tuweke dawa mapema tutumie viuatilifu ambavyo vinashauriwa na wataalamu wa kilimo, baada ya hpo tuangalie mashamba yetu kwa kupalilia kwa kufanya hivi tunaweza kuzidfi hata gunia 20 kwa ekari,” Alisema.

Ameyasema hayo alipokuwa katika ziara yake maalum ya kuhamasisha kilimo chenye tija katika Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Mkoani humo akiwa pamoja na wataalamu wa kilimo wa mkoa na halmashauri pamoja na mkuu wa Wilaya hiyo.

Kwa upande wao mmoja wa wamiliki wa shamba lililotembelewa na Mkuu wa Mkoa Bwana Rojas Lukas amesema kuwa changamoto ubwa inayowakuta wakulima na kushindwa kuendelea kulima kilimo chenye tija ni mitaji pamoja na mdudu mharibifu aina ya kiwavi jeshi.

“Kuna mdudu Fulani anaitwa Kiwavi jeshi Yule anatusumbua sananingeomba serikali ijaribu kututafutia dawa ambayo inaweza ikamuua Yule mdudu, kingine tunaomba serikali itusaidie kama inawezekana watukopeshe ili tukuze kilimo chetu kiende mbele,” Alisema.

Akimkaribisha Mkuu wa mkoa katika shamba la mmoja wa wakulima hao mkuu wa Wilaya ya Kalambo Mh. Juliet Binyura alisema kuwa watalaamu wameendelea kutoa ushauri kwa wananchi mbalimbali na hivyo kuwaomba kuendelea kufanya hivyo ili kuwasaidia wakulima kuweza kufikia kilimo chenye tija.

“Tumekuja kuangalia utaalamu aliopewa kwa wataalamu ambao ni maafisa ugani katika kata yake na wanapanda kwa kutumia kamba na wanapima vipimo vinavyokubalika naamini ya kwamba mazao atavuna vizuri,” Alisema.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa