• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wanarukwa wahamasishwa kuujaza uwanja wa Mandela mechi ya Tanzania Prison na Namungo

imewekwa Tar: September 18th, 2020

Viongozi mbalimbali mkoani Rukwa wamejitokeza kuwahamasisha wananchi mkoani humo kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi katika mechi ya kwanza ya Ligi Kuu ya Vodacom kwa mkoa huo itakayochezwa katika Uwanja wa Nelson Mandela mjini Sumbawanga kati ya timu ya Tanzania Prison iliyohamishia makazi yake mjini Sumbawanga dhidi ya timu ya Namungo yenye makazi yake Wilayani Ruangwa Mkoani Lindi.

Wakiongea katika nyakati mbali mbali pindi walipotembelea kuona maandalizi ya uwanja huo kwaajili ya mechi hiyo wamesema kuwa hakika mechi hiyo itakuwa ni ya kihistoria katika mkoa wa Rukwa ambao hakuna timu hata moja ambayo imeshawahi kushiriki ligi kuu kwa Zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Akiongea kwa niaba ya kamati maalum ya Mkoa inayoshughulika na kuilea timu katika Mkoa huo Mwenyekiti wa Kamati hiyo Dkt. Chrisant Mzindakaya aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu hiyo ambayo kwa sasa ndio timu ya nyumbani kwa watu wa mkoa huo.

“Timu hii ni mali yetu, si ya magereza tena, kwa jina timu ya magereza lakini kwa vitendo ni timu ya mkoa huu wa Rukwa itakuwa hapa siku zote, tutakuwa nao siku zote, mpira ambao utacheza keshi ni na Namungo, Namungo haiwezi kuwashinda magereza, lakini kubwa kuliko yote ni ninyi wananchi wa Sumbawanga hap ana vitongoji vyote mfike mshuhudie mchezo mzuri utaofanyika hapo kesho, tunaamini kiwango kilichowekwa cha kuingia hapa uwanjani ni cha kusaidia watu wengi muingie,” Alisema.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu mkoa wa Rukwa Blasi Kiondo aliwaalika wadau wote wa mpira wa ndani ya mkoa na wilaya zake pamoja na mikoa ya jirani ikiwemo Mkoa wa Songwe na Katavi kufika katika Uwanja wa Nelson Mandela kushuhudia mpamabano huo na kuongeza kuwa kutakuwa na mechi ya utangulizi ya vijana chini ya miaka 17 itakayoanza saa 5 mchana kabla ya mechi hiyo ya ligi kuu.

“Kiingilio chetu ni rahisi sana, tumeweka kiingilio cha Shilingi Elfu tatu kwa mzunguko wa uwanja mzima na tumeweka shilingi elfu saba kwa VIP, na nitangazie wanachi wote kuwa kuingia mapema ni vizuri Zaidi kwasababu kutakuwa na mechi chini ya umri wa miaka 17 itakayoanza saa tano mpaka saa sita mchana,” Alisema.

Kwa upande wake Katibu mkuu wa Tanzania Prisons Jabu Adam Kifukwe aliwahakikishia wadau wote wa mpira mkoani humo kuwa timu yao imejiandaa vyema kwaajili ya mechi hiyo ya nyumbani na wasiwe na shaka juu ya wachezaji kwamba wote wapo katika afya njema na hakuna mwenye majeraha na kuomba wananchi wajitokeze kwa wingi katika kuishangilia timu hiyo.

“Waje watupe support, kwamba bila ya wao sisi tunajua kwamba wao ndio wachezaji namba 12 wanaipa Support kubwa waje waiunge mkono timu yao, tupo nyuma yao watuongoze tuweze kushinda mechi hii,” Alimalizia.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa ACP Justin Masejo amewahakikishia wananchi ulinzi na usalama kuanzia maandalizi ya mechi hiyo, kuanza kwa mechi hadi kumalizika kwake. 

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa