• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

WanaRukwa Wahimizwa kulima Kahawa ili kuwa zao mbadala la biashara.

imewekwa Tar: January 22nd, 2018

Wakulima wa mkoa wa Rukwa wamehimizwa kuona namna ya kujiwekeza katika kilimo cha kahawa ili kupata zao mbadala la biashara kuliko kubaki katika zao moja la mahindi ambalo mara nyingine huwa na shida ya kupanda na kushuka kwa bei kusikotabirika.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachima Wangabo alipotembelea kikundi cha watu 56 cha wakulima wa zao hilo katika Kijiji cha Katuka, Kata ya Msanzi, Wilayani Kalambo ikiwa ni miongoni mwa kuwatia moyo wakulima hao wachache ili wawe mfano kwa wakulima wengine na kuwasihi kuanzisha ushirika ili kuweza kupata soko.

Mh. Wangabo amesema kuwa kuwa kahawa huvunwa kila mwaka na kupandwa mara moja na kufanyiwa marekebisho madogo madogo pamoja na kuweza kuchanganya na baadhi ya mazao mengine ndani ya shamba moja tofauti na zao la mahindi ambalo hupandwa kila mwaka na kuongeza kuwa Serikali imejipanga kufufua zao la kahawa kwa nguvu zote.

“Changamoto ya soko serikali imeitafutia ufumbuzi, soko la kahawa litapitia kwenye Ushirika na linaenda kuuzwa kwa njia ya mnada kama inavyofanyika katika zao la korosho, kwa hali hiyo hakutakuwa na changamoto kubwa inayotarajiwa kwa zao hilo, kinachotakiwa ni kuimarisha ushirika wa kahawa” Alisema na kuongeza kuwa kama Mkoa utakuwa na Chama kikuu cha Ushirika cha kahawa.

Akisoma risala mbele ya Mh. Wangabo, Mkuu wa Idara ya kilimo Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Nicholas Mlango amesema kuwa halmashauri imeandaa kozi kwaajili ya wakulima wa kahawa na wataalamu kuendelea kuwaelimisha wakulima juu ya kujiunga na mfuko wa kahawa wataochangia ili kukuza mfuko huo.

Nae mmoja wa wakulima waliotembelewa shamba lake John Kapalata alisema kuwa changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni kutokuwa na vifaa  na elimu ya kutosha kuweza kutunza mashamba hayo ya kahawa japo wana nia ya kuendeleza kilimo hicho jambo lililopelekea Mkurugenzi wa halmashauri hiyo James Ngagani kuahidi kuwapeleka wakulima 20 wa zao hilo katika mafunzo Wilayani Mbozi na kutoa miche 30,000 bure kwa wananchi wanaohitaji kulima zao hilo.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa