• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

WanaRukwa Wahimizwa kulima Kahawa ili kuwa zao mbadala la biashara.

imewekwa Tar: January 22nd, 2018

Wakulima wa mkoa wa Rukwa wamehimizwa kuona namna ya kujiwekeza katika kilimo cha kahawa ili kupata zao mbadala la biashara kuliko kubaki katika zao moja la mahindi ambalo mara nyingine huwa na shida ya kupanda na kushuka kwa bei kusikotabirika.

Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachima Wangabo alipotembelea kikundi cha watu 56 cha wakulima wa zao hilo katika Kijiji cha Katuka, Kata ya Msanzi, Wilayani Kalambo ikiwa ni miongoni mwa kuwatia moyo wakulima hao wachache ili wawe mfano kwa wakulima wengine na kuwasihi kuanzisha ushirika ili kuweza kupata soko.

Mh. Wangabo amesema kuwa kuwa kahawa huvunwa kila mwaka na kupandwa mara moja na kufanyiwa marekebisho madogo madogo pamoja na kuweza kuchanganya na baadhi ya mazao mengine ndani ya shamba moja tofauti na zao la mahindi ambalo hupandwa kila mwaka na kuongeza kuwa Serikali imejipanga kufufua zao la kahawa kwa nguvu zote.

“Changamoto ya soko serikali imeitafutia ufumbuzi, soko la kahawa litapitia kwenye Ushirika na linaenda kuuzwa kwa njia ya mnada kama inavyofanyika katika zao la korosho, kwa hali hiyo hakutakuwa na changamoto kubwa inayotarajiwa kwa zao hilo, kinachotakiwa ni kuimarisha ushirika wa kahawa” Alisema na kuongeza kuwa kama Mkoa utakuwa na Chama kikuu cha Ushirika cha kahawa.

Akisoma risala mbele ya Mh. Wangabo, Mkuu wa Idara ya kilimo Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo Nicholas Mlango amesema kuwa halmashauri imeandaa kozi kwaajili ya wakulima wa kahawa na wataalamu kuendelea kuwaelimisha wakulima juu ya kujiunga na mfuko wa kahawa wataochangia ili kukuza mfuko huo.

Nae mmoja wa wakulima waliotembelewa shamba lake John Kapalata alisema kuwa changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni kutokuwa na vifaa  na elimu ya kutosha kuweza kutunza mashamba hayo ya kahawa japo wana nia ya kuendeleza kilimo hicho jambo lililopelekea Mkurugenzi wa halmashauri hiyo James Ngagani kuahidi kuwapeleka wakulima 20 wa zao hilo katika mafunzo Wilayani Mbozi na kutoa miche 30,000 bure kwa wananchi wanaohitaji kulima zao hilo.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa