• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wanarukwa watolewa mashaka kuhusu Ebola.

imewekwa Tar: May 22nd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatoa mashaka wanarukwa juu ya kutokuwepo kwa ugonjwa wa Ebola katika Mkoa na kutahadharisha yeyote anaejaribu kuleta hofu ya ugonjwa huo katika Mkoa na kuwataka wananchi wasijengewe hofu bali waendelee kuchukua hatua za tahadhari za kujikinga na ugonjwa huo.

Amesema kuwa Mkoa unaendelea kushirikiana na sekta mbalimbali katika kuimarisha ufuatiliaji na kutekeleza mikakati ya udhibiti ikiwemo kutoa taarifa na elimu kwa jamii kwa kadiri itakavyohitajika ili ugonjwa huo usiingie katika mkoa.

“Katika kipindi hiki ambacho tunatakiwa kuchukua tahadhari kubwa, wananchi wote wa Mkoa wa Rukwa ni lazima tuwe na mshikamano, umoja na tahadhari kubwa sana na hasa maeneo yale ya Ziwa Tanganyika ambako kuna muingiliano wa watu kutoka Zambia, DRC, Rwanda na Burundi. Lakini pia wanaotokea maeneo mengine ya nchi, la muhimu ni kuchukua tahadhari kubwa sana,” Alisema

 Ameongeza kuwa wenyeviti wa vijiji wajizatiti katika kuboresha taarifa za wakazi wao kwenye madaftari yao na kuwa makini na wageni wanaoingia kwenye maeneo yao pamoja na kuitaka idara ya uhamiaji kuhakikisha wageni wote wanaingia katika njia zilizo rasmi.

Ameyasema hayo alipokuwa akifungua kikao cha wadau wa afya Mkoa kilichoitishwa na Mganga Mkuu wa mkoa ili kutoa elimu kwa wawakilishi wa makundi mbalimbali ya jamii ikiwemo waandishi wa habari juu kusambaza ujumbe huo wa kujihadhari na ugonjwa huu hatari wa Ebola.

Mmoja wa wadau hao akiwakilisha kundi la wazee, Zeno Nkoswe amesema kuwa serikali ya Mkoa haina budi kuhakikisha elimu hiyo inafikishwa kwa viongozi wote wa dini kwani wao wanauwezo wa kuwafikia wananchi wengi zaidi na kwa muda ufupi na ujumbe hatimae kutimiza malengo ya kufisha ujumbe huo kwa wananchi.

Akichangia mjadala huo mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mkoa wa Rukwa, Sadrick Malila amesema kuwa serikali haina budi kutumia redio zilizopo Mkoani Rukwa ili kufikisha ujumbe huo kwa watu wote na maeneo yote ya Mkoa na mikoa ya jirani ili watu waweze kujikinga na ugonjwa huo.

Ugonjwa wa Ebola upo katika nchi ya jirani ya Jamhuriya watu wa Kongo katika mji wa Biroko, jimbo la Equator na kwa taarifa za shirika la afya duniani, hadi kufikia tarehe 17 Mei, 2018 watu 44 walikuwa wamebainika kuwa na ugonjwa huo na watu 23 kufariki.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE( CSEE) 2025 January 31, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO SUMBAWANGA; ASISITIZA UMUHIMU WA HATI MILIKI ZA MAENEO YA TAASISI

    January 29, 2026
  • UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO; RC MAKONGORO AHIMIZA UBORA NA KUZINGATIWA KWA MUDA WA UTEKELEZAJI NKASI DC

    January 28, 2026
  • KUMBUKIZI YA KUZALIWA RAIS SAMIA; RC MAKONGORO AMUUNGA MKONO KWA KUONGOZA WANANCHI RUKWA KUPANDA MITI 4565

    January 27, 2026
  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa