• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wanawake Rukwa watajiwa wanaowarudisha nyuma kimaendeleo

imewekwa Tar: March 8th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatambulisha rasmi wakurugenzi wa halmashauri mbili za mkoa huo wanaochangia kukwamisha maendeleo ya wanawake katika halmashauri zao huku akiwataka wakurugenzi wawili wengine kuhakikisha wanamaliza asilimia nne ya mikopo kwa wanawake kabla ya kuisha kwa mwaka wa fedha 2019/2020.

Amesema kuwa katika halmashauri nne za mkoa huo ni Manispaa ya Sumbawanga pekee ndio inayoongoza kwa utoaji wa mikopo hiyo ikifuatiwa na halmashauri ya Wilaya Kalambo huku halmashauri ya Wilaya ya Nkasi pamoja na halmashauri ya Wilaya ya Sumbanga zikiwa hazina dalili za kufikia lengo hilo hali iliyompelekea Mkuu huyo wa Mkoa kuwasimamisha ili wanawake waliohudhuria kwenye maadhimisho ya siku ya wanawake duniani kuwatambua.

“Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga 4% kati ya 10% inayotakiwa kutolewa kwa wanawake ni shilingi Milioni 86, lakini halmashauri hii imetoa shilingi milioni 10 peke yake, sasa hii haifurahishi walipaswa hadi kufikia sasa kufikia shilingi milioni 45 wawe wamevuka nusu ile inayotakiwa lakini wametoa shilingi milioni 10 tu, kwahiyo mtu anayewaangamiza na anayewadidimiza wanawake katika halmashauri zenu mnaanza kumuelewa mbaya wenu ni halmashauri gani, halmashauri ya Sumbawanga DC hii ndio hali waliyonayo inamaana hawawajali hawa wanawake pamoja na kwamba tunayo sheria inayobana kutekeleza hayo maagizo,” Alisema.

Mh. Wangabo aliongeza kuwa nayo halmashauri ya Nkasi ilitakiwa kutoa shilingi milioni 87 lakini imetoa shilingi milioni 10 tu huku ikisajili vikundi 130 na kuvipa mikopo vikundi 2 vyenye wanufaika 45 wakati Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ikiwa imesajili vikundi 122 na kutoa mikopo kwa vikundi 3 vyenye wanufaika 63.

“Nitoe rai kwa wakurugenzi wa Halmashauri zote za mkoa wa Rukwa kuhakikisha kwamba hadi kufikia mwishoni mwa mwezi Juni, 2020 fedha zote zilizobaki ziwe zimetolewa vinginevyo watajikuta pabaya na kujikuta wanalia na kusaga meno, huu sio mchezo kwasababu hizi fedha ni za kisheria, kama hutekelezi hii sheria na wakumbuke kuwa huku nyuma kuna madeni ambayo hawakufikia 10% ikiwemo 4% kwa wanawake, 4% kwa vina na 2% kwa watu wenye ulemavu,” Alisema.

Mh. Wangabo aliyasema hayo katika maadhimisho ya kilele cha siku ya wanawake duniani ambayo hufanyika kila ifikapo tarehe 8 Machi ambapo kimkoa ilifanyika katika viwanja vya Kijiji cha Kisumba, kata ya Kisumba, Wilayani Kalambo akijibu risala iliyosomwa na jukwaa la uwezeshaji wanawake kiuchumi katika mkoa huo.

Aidha, amewataka wakurugenzi hao kuhakikisha wanatenga bajeti ya kuyawezesha majukwaa ya wanawake katika halmashauri zao ili kuweza kurahisisha shughuli za majukwaa hayo ambapo katika sherehe hizo aliweza kulizindua jukwaa la wanawake la halmashauri ya wilaya ya Kalambo.

Wakati akisoma risala mbele ya mgeni rasmi wa maadhimisho hayo kimkoa Katibu wa Jukwaa la Uwezeshaji kiuchumi Mkoa wa Rukwa Bi.Leonora Jailos alisema kuwa wanawake wa mkoa wa Rukwa wako mstari wa mbele katika shughuli za kilimo na hivyo kujipanga katika kufikia Tanzania ya viwanda kwa kuanzisha viwanda vidogo ikiwemo vya kusindika vyakula na mazao na kueleza kuwa miongoni mwa changamoto wanazopata ni fedha kidogo za mikopo wanazopatiwa na halmashauri.

“Baadhi ya changamoto tulizonazo wanawake wa Mkoa wa Rukwa ni kwamba, moja mikopo ya 4% tunayopewa na halmashauri zetu kwenye vikundi, ni fedha kidogo ambazo hazituendelezi tulivyojipanga ili kutuendeleza kiuchumi, hivyo basi tunaiomba serikali kuangalia namna nyingine kiasi cha fedha kinachotolewa kama mikopo, vile vile wanawake tukopeshwe vifaa kulingana na shughuli za kikundi,” Alisema

Katika hatua nyingine, Mkuu wa Mkoa huyo amesema kuwa Mkoa umeendelea kupambana na tatizo la ukatili wa kijinsia na mimba za utotoni kwa kuzindua mkakati wa kimkoa wa kukabiliana na mimba za utotoni kwa lengo la kuhakikisha mtoto wa kike anapata fursa ya kuendelea na masomo yake hadi chou kikuu huku akiwaonya wanaume wenye tabia ya kuwanyanyasa wanawake hasa katika msimu wa mavuno kwa kuuza mazao yote wakati kwenye shughuli za kilimo hakushiriki ipasavyo na matokeo yake hujinufaisha na kuiacha familia katika hali mbaya.

Katika maadhimisho hayo ambayo Manispaa ya Sumbawanga iliweza kung’ara kwa kutokana na rekodi yake ya kutoa shilingi milioni 90 kati ya 165.8 ya 4% ya mikopo kwa wanawake huku ikiwa imesajili vikundi 322 na kutoa mikopo kwa vikundi 138 huku idadi ya wanufaika ikiwa ni wanawake 863 na kauli mbiu ya maadhimisho hayo ni “Kizazi cha Usawa kwa Maendeleo ya Tanzania ya Sasa nay a Baadaye”. 

 

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa