• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

wasichana zaidi ya 26,000 kupata chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi, Rukwa.

imewekwa Tar: April 17th, 2018

Zaidi ya Wasichana 26,000 wenye umri wa miaka 14 wanatarajia kupatiwa chanjo ya kuzuia saratani ya mlango wa kizazi mkoani Rukwa ikiwa ni juhudi za serikali ya mkoa kuwakinga wasichana hao kutokana na madhara makubwa yanayoweza kuwapata pindi wanapofikia umri wa utu uzima.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo alipokuwa akifungua kikao cha wadau wa chanjo ngazi ya mkoa kwaajili ya maandalizi ya utoaji wa chanjo mpya ya kinga dhidi ya saratani ya mlango wa kizazi kwa wanawake mkoani Rukwa.

 “Kwa Mkoa wetu wa Rukwa, jumla ya wasichana 26,234 wanatarajiwa kupatiwa chanjo hii muhimu, Wazazi na Walezi, wahakikishe kuwa watoto wa umri wa miaka 14 wanaenda katika vituo vya kutolea huduma za chanjo kupata chanjo. Naomba kuwahakikishia wananchi kuwa chanjo zinazotolewa katika vituo vyetu ni salama na zinatolewa na wataalamu wenye uzoefu waliopatiwa mafunzo,” Alisema.

 

Nae Mganga mkkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu amesema kuwa zoezi hilo linatarajiwa kuanza katika wiki ya mwisho wa mwezi wanne ambayo itakuwa ni wiki ya chanjo ya saratani ya mlango wa kizazi kwa nchi nzima ambapo uzinduzi wake ulifanyika tarehe 10, Aprili mwakahuu

 Pia ametaja sababu kadhaa zinazosababisha ugonjwa huo ikiwemo watoto wa kike kushiriki tendo la ndoa wakiwa katika umri mdogo, kuwa na wapenzi wengi, uvutaji wa sigara na kuonya kuwa dalili zake hujitokeza baada ya saratani hiyo kusambaa mwilini.

“Baadhi ya dalili za saratani ya mlango wa kizazi ni pamoja na kutokwa damu ya hedhi bila mpangilio, kutokwa damu baada ya tendo la ndoa, maumivu ya mgongo, miguu na/au kiuno, kuchoka, kupungua uzito, kukosa hamu ya kula, kutokwa uchafu wa rangi ya kahawia au wenye damu ukeni na kuvimba miguu,”Alisema.

Kwa upande wao mwakilishi wa viongozi wa dini ambae ni katibu wa Bakwata Mkoani Rukwa Mohamed Adam amesema kuwa kama viongozi wa dini watahakikisha wanakuwa mstari wa mbele katika kuwahamasisha waamini wao kujiunga na juhudi za serikali katika kupunguza vifo vinavyosababishwa na saratani ya mlango wa kizazi.

Imeelezwa kuwa, nchini Tanzania zaidi ya asilimia 36 ya wagonjwa wa saratani wanaugua saratani ya mlango wa kizazi ikiwa na wastani wa wagonjwa 51 kwa kila kinamama 100,000, na kuongoza kwa kusababisha vifo ikifuatiwa na saratani ya matiti ambazo kwa pamoja husababisha zaidi ya asilimia 50 ya vifo vyote vya akina mama vitokanavyo na saratani.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa