• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Watendaji watakiwa kuwa na idadi kamili ya wanafunzi walemavu na wanaopatiwa msaada

imewekwa Tar: December 11th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka maafisa Ustawi wa Jamii Mkoani humo kuainisha idadi kamili ya wananfunzi wenye ulemavu wa aina mbalimbali katika shule za Msingi na Sekondari na namna wanavyosaidiwa katika kusaidiwa kupata elimu kulingana na mazingira yao.

Mh. Wangabo amesema kuwa kwa muda mrefu serikali imekuwa ikiwahamasisha wazazi kutowaficha watoto wenye ulemavu kwa kuwapeleka shule lakini takwimu za kimsaada kwa Watoto hao hazijulikani kwa wazazi wengine ambao bado wanawaficha Watoto wao wakidhani kuwa hawapatiwi msaada stahiki.

“Kwasababu akimpeleka shule kuna changamoto kubwa, kuna mwenye ulemavu wa viungo lakini hana vifaa saidizi atafanyaje? Lakini tukijielekeza kuwasaidia hawa ambao wako mashuleni basi na wale ambao wako majumbani watahamasika sasa kuwapeleka shuleni kwasababu tayari sasa wana vifaa saidizi, wanaona kabisa jamii inawajali, mashirika makampuni yanawajali, kwahiyo wakati tunasema Watoto wenye ulemavu wasifichwe watolewe waende shule basin a wale waliopo shule tuwafahamu, tuwasadidie ili na wale wengine waweze kuona jamii sasa inawajali,” Alisisitiza.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa saidizi kwa viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) Pamoja na Chama cha Walemavu Tanzania (CHAWATA) vilivyotolewa na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC PLC).

Wakati akitoa taarifa fupi ya hali ya watu wenye ulemavu mkoani humo Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Rukwa Godfrey Mapunda alisema kuwa kuanzia mwaka 2019 hadi 2020 mkoa umetambua jumla ya watu wenye ulemavu 1,616 ambao kati ya hao wenye umri chini ya miaka 18 ni 574 na wenye umri wa Zaidi ya miaka 18 ni 1,042 huku wanaume wakiwa 923 na wanawake 693.

Kwa upande wake mwakilishi wa Kampuni ya Sigara Tanzania Oscar Lwoga alisema kuwa kampuni hiyo imewasilisha baiskeli za miguu mitatu 10, fimbo nyeupe 61 na magongo 74 kwaajili ya kusaidia sehemu ndogo ya wahitaji wa vifaa hivyo saidizi katika mkoa wa Rukwa.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE( CSEE) 2025 January 31, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO SUMBAWANGA; ASISITIZA UMUHIMU WA HATI MILIKI ZA MAENEO YA TAASISI

    January 29, 2026
  • UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO; RC MAKONGORO AHIMIZA UBORA NA KUZINGATIWA KWA MUDA WA UTEKELEZAJI NKASI DC

    January 28, 2026
  • KUMBUKIZI YA KUZALIWA RAIS SAMIA; RC MAKONGORO AMUUNGA MKONO KWA KUONGOZA WANANCHI RUKWA KUPANDA MITI 4565

    January 27, 2026
  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa