• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Watendaji watakiwa kuwa na idadi kamili ya wanafunzi walemavu na wanaopatiwa msaada

imewekwa Tar: December 11th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka maafisa Ustawi wa Jamii Mkoani humo kuainisha idadi kamili ya wananfunzi wenye ulemavu wa aina mbalimbali katika shule za Msingi na Sekondari na namna wanavyosaidiwa katika kusaidiwa kupata elimu kulingana na mazingira yao.

Mh. Wangabo amesema kuwa kwa muda mrefu serikali imekuwa ikiwahamasisha wazazi kutowaficha watoto wenye ulemavu kwa kuwapeleka shule lakini takwimu za kimsaada kwa Watoto hao hazijulikani kwa wazazi wengine ambao bado wanawaficha Watoto wao wakidhani kuwa hawapatiwi msaada stahiki.

“Kwasababu akimpeleka shule kuna changamoto kubwa, kuna mwenye ulemavu wa viungo lakini hana vifaa saidizi atafanyaje? Lakini tukijielekeza kuwasaidia hawa ambao wako mashuleni basi na wale ambao wako majumbani watahamasika sasa kuwapeleka shuleni kwasababu tayari sasa wana vifaa saidizi, wanaona kabisa jamii inawajali, mashirika makampuni yanawajali, kwahiyo wakati tunasema Watoto wenye ulemavu wasifichwe watolewe waende shule basin a wale waliopo shule tuwafahamu, tuwasadidie ili na wale wengine waweze kuona jamii sasa inawajali,” Alisisitiza.

Mh. Wangabo ameyasema hayo katika hafla fupi ya kukabidhi vifaa saidizi kwa viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Watu wenye Ulemavu Tanzania (SHIVYAWATA) Pamoja na Chama cha Walemavu Tanzania (CHAWATA) vilivyotolewa na Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC PLC).

Wakati akitoa taarifa fupi ya hali ya watu wenye ulemavu mkoani humo Afisa Ustawi wa Jamii Mkoa wa Rukwa Godfrey Mapunda alisema kuwa kuanzia mwaka 2019 hadi 2020 mkoa umetambua jumla ya watu wenye ulemavu 1,616 ambao kati ya hao wenye umri chini ya miaka 18 ni 574 na wenye umri wa Zaidi ya miaka 18 ni 1,042 huku wanaume wakiwa 923 na wanawake 693.

Kwa upande wake mwakilishi wa Kampuni ya Sigara Tanzania Oscar Lwoga alisema kuwa kampuni hiyo imewasilisha baiskeli za miguu mitatu 10, fimbo nyeupe 61 na magongo 74 kwaajili ya kusaidia sehemu ndogo ya wahitaji wa vifaa hivyo saidizi katika mkoa wa Rukwa.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa