• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

imewekwa Tar: December 17th, 2025

Watumishi wa sekta ya afya mkoani Rukwa wamehimizwa kuendelea kutoa elimu na hamasa kwa wananchi ili kuongeza uelewa na ushiriki wao katika mpango wa Bima ya Afya kwa Wote, unaolenga kuhakikisha kila mwananchi anapata huduma bora za afya bila vikwazo vya kifedha. 

Wito huo umetolewa leo tarehe 17 Desemba 2025, katika kikao cha Mfuko wa Bima ya Taifa kilichowakutanisha wataalamu wa afya kutoka vituo mbalimbali vya kutolea huduma mkoani humo.Kikao hicho kililenga kujadili namna bora ya kuimarisha utekelezaji wa mpango huo ngazi ya jamii.

 Akizungumza katika kikao hicho kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Katibu Tawala wa Mkoa,Ndugu Robert Msalika Makungu, amesema kuwa uelewa wa wananchi kuhusu Bima ya Afya kwa Wote ni jambo la msingi katika kufanikisha dhamira ya Serikali ya kutoa huduma za afya zilizo nafuu, endelevu na zinazopatikana kwa wakati.

 

Ameeleza kuwa wananchi wengi hukumbwa na changamoto ya kugharamia huduma za afya pindi wanapopatwa na magonjwa ya ghafla au dharura,hali inayoweza kusababisha kuchelewa au kushindwa kabisa kupata matibabu stahiki.Kupitia Bima ya Afya kwa Wote,wananchi wataweza kupata huduma muhimu za afya bila kulazimika kubeba mzigo mkubwa wa kifedha wakati wa uhitaji. “Watumishi wa afya mna nafasi ya kipekee ya kuwafikia wananchi moja kwa moja.Elimu mnayotoa siyo tu kuhusu matibabu, bali pia kuhusu kinga na maandalizi ya kifedha kwa afya zao,”amesema Ndugu Msalika. 

Amehimiza matumizi ya njia jumuishi za mawasiliano ikiwemo mikutano ya hadhara,vikao vya kijamii, nyumba za ibada na majukwaa ya mitandao ya kijamii ili ujumbe kuhusu umuhimu wa kujiunga na bima ya afya uwafikie wananchi wengi zaidi kwa lugha rahisi na inayoeleweka. 

Aidha,amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuhakikisha kaya maskini zinatambuliwa kwa haki na usahihi ili ziweze kunufaika na mpango wa kulipiwa bima ya afya, hatua inayolenga kulinda utu wa mwananchi na kuhakikisha hakuna anayebaki nyuma katika kupata huduma za afya. Kwa ujumla, kikao hicho kimeweka msisitizo kwamba elimu ya bima ya afya si jukumu la Serikali pekee, bali ni wajibu wa pamoja unaohitaji ushiriki wa jamii.


Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa