• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wawili wakamatwa, mmoja afutiwa mkataba ujenzi wa hospitali ya Wilaya.

imewekwa Tar: April 18th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kusitisha mkataba na fundi anayehusika na ujenzi wa jengo la maabara katika ujenzi wa hospitali ya Wilaya ya Kalambo huku akimtaka Mkurugenzi huyo kutafuta chumba katika eneo hilo ili asimamie kwa karibu ujenzi unaoendelea na kuhakikisha unaisha kwa wakati.

Ametoa maagizo hayo ikiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Waziri wa Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mh. Suleiman Jafo hivi karibuni baada ya kuitaka mikoa yote kusimamia ujenzi wa hospitali za wilaya na kufikia tarehe 13 hadi 25 Mei, 2019 majengo yote yawe yameshapauliwa na mikoa hiyo kutuma picha za majengo saba ya hospitali hizo.

Kwa kutekeleza hayo Mh. Wangabo amewaagiza mafundi wote wanaosimamia ujenzi wa majengo hayo saba kuhakikisha wanafikia usawa wa linta ifikapo tarehe 10 mwezi Mei mwaka huu na hatimae kumalizika kwa wakati.

Mh. Wangabo ameyasema hayo alipotembelea eneo la ujenzi wa hospitali ya wilaya ya Kalambo na kukutana na wataalamu wa halmashauri wakiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri hiyo Msongela Palela pamoja na mafundi waliopewa mkataba kwaajili ya ujenzi wa hospitali.

Baada ya kutembelea alisema kuwa hakuridhishwa na kasi ya ujenzi wa hospitali hiyo ya Wilaya ya Kalambo kwakua kasi ni ndogo pamoja na kujua kuwa kulikuwa na changamoto nyingi hasa kipindi cha mvua ambapo barabara zilikuwa hazipitiki hivyo vifaa mbalimbali kushindwa kufika kwenye eneo la ujenzi na kutahadharisha kuwa sasa mvua zimeisha hivyo hakuna sababu ya kuendelea na kasi ile iliyokuwepo.

“Lakini pia nimegundua kuwa kuna wajenzi wengine hata ‘saiti’ hawapo na ujenzi wa majengo yao unasuasua, sasa yule mjenzi wa maabara kule Mkurugenzi sitisha mkataba wake mara moja na utafute mjenzi mwengine ambaye ataleta mafundi wengi na hili jambo lichukue muda mfupi iwezekanavyo ili tarehe 10 mwezi Mei majengo yote haya saba yawe yamefika kwenye hatua ya linta na sio vinginevyo,” alisisitiza.

Halikadhalika, alisikiliza kilio cha vibarua wanaoendelea na ujenzi wa majengo ya hospitali hiyo na kugundua kuwa kuna kusuasua kwa malipo ya vibarua hao na hivyo kumuagiza Kamanda wa polisi wa Wilaya hiyo kuwakamata fundi anayehusika na ujenzi wa jengo la utawala Fadhili Salum pamoja na msaidizi wake Amir Rajabu kwa kushindwa kuwalipa vibarua wao tangu ujenzi huo uanze mwanzoni mwaka huu na kumtaka Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kufuatilia malipo ya vibarua hao kwa karibu ili wasiharibu kazi.

Serikali imetoa jumla ya Shilingi bilioni 105 kwa wilaya 67 kwaajili ya utekelezaji wa ujenzi wa hospitali za wilaya ambapo kila Wilaya ilipewa Shilingi bilioni 1.5 kwaajili ya ujenzi wa majengo saba ya hospitali hizo ambapo mwisho wa ujenzi huo na majengo hayo kuanza kutumika ni tarehe 30 June, 2019.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa