• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

WAZIRI LUGOLA AWATUMBUA MKUU WA POLISI WILAYA, OC CID, OCS NKASI

imewekwa Tar: October 4th, 2019

Na Mwandishi Wetu, MOHA, Nkasi

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola amewaondoa katika nyadhifa zao viongozi wakuu wa Jeshi la Polisi wa Wilaya ya Nkasi, Mkoani Rukwa kwa kushindwa kumudu majukumu yao baada ya kubaini kuwepo kwa wizi wa mara kwa mara wa mifugo wilayani humo.

Lugola pia ameagiza askari sita wa Kituo cha Polisi Namanyere na Kirando wilayani humo waondolewe kutokana na wananchi wengi wanawalalamikia kwa kushindwa kuwasaidia wanaporipoti matukio mbalimbali vituoni uwapuuza na kuwakatisha tamaa.

Akizungumza na wananchi katika Mkutano wa hadhara, mjini Namanyere, Wilayani humo, Lugola alisema Mkuu wa Polisi wa Wilaya hiyo (OCD), David Mtasya, Mkuu wa Upelelezi wa Wilaya (OC CID), Emanuely Kajala na Mkuu wa Kituo cha Polisi Namanyere (OCS) Wilayani humo, Ramadhani Msangi, lazima waondoke katika Wilaya hiyo kwa kuwa wameshindwa kuimudu kazi yao ipasavyo.

“Wananchi wa Namanyere, kufuatia malalamiko yaliyowasilishwa mkutanoni hapa na wamelalamikia kama mlivyowasikia kutopata msaada kutoka kwa Jeshi la Polisi pindi wanalipotoa mara kwa mara taarifa ya kuibiwa ng’ombe 278 za wamiliki tofauti katika kituo cha polisi lakini hawasikilizwi, wanazungushwa, wanapuuzwa mpaka kiasi kikubwa cha ng’ombe kimepotea, licha ya kuwa wananchi 15 walioripoti polisi na mpaka sasa hawajapata msaada wa polisi, hii haiwezekani na siwezi kukaa kimya, viongozi hawa wameshindwa kazi, na lazima waondoke waje wengine,” alisema Lugola.

Aliongeza kuwa, licha ya polisi hao kupokea malalamiko mengi vituoni, lakini wanawaachia watuhumiwa hao wanaotuhumiwa kuiba ng’ombe za wananchi, na pia uonekana mitaani kiasi kwamba wananchi hao wanapatwa na hasira na kuanza kuichukia serikali.

Akitoa kero yake kwa Waziri huyo, mkazi wa Namanyere, wilayani Nkasi, Felista Mkomo, alisema mwaka jana aliibiwa ng’ombe wake lakini walifanikiwa kuwakamata wawili ila wengine mpaka sasa hawajawapata, hata hivyo aliripoti tukio hilo kituo cha polisi lakini mpaka sasa hakuna chochote kilichofanyika na hakuna wezi aliyekamatwa.

“Mheshimiwa Waziri mimi kero yangu ni wizi wa ng’ombe, niliibiwa mwaka jana, katika kuwatafuta nikafanikiwa kuwapata wawili, lakini nikaamua kwenda polisi kuripoti tukio hili la wizi, mpaka sasa hakuna taarifa zozote na sijawapata ng’ombe wangu,” alisema Felista.

Aliongeza kuwa Polisi hao wameshindwa kuwasaka mitaani watuhumiwa hao wa wizi, kiasi kwamba wizi unaendelea wilayani humo na uwafanya kukosa mahali pa kukimbilia kutoa malalamiko yao.

Waziri Lugola akijibu kero hizo, alisema Serikali ya Dkt. Magufuli haiwezi kuchezewa na mtu yeyote, na kamwe haiwezi kuona wananchi wake wanateseka kiasi hicho, viongozi wa polisi wilaya wameshindwa kumudu kazi zao, wameshindwa kuwahudumia wananchi, hivyo polisi hao wanapaswa kuondoka wilayani humo, na wataletwa wapya.

Aidha, Waziri Lugola alilitaka Jeshi la Polisi mkoani humo, kuwasaka wazazi na walezi ambao wanawatumikisha watoto wao kufanya kazi katika Ziwa Tanganyika badala ya kuwapeleka shule na kuendelezea wimbi la umaskini katika maeneo mbalimbali ya ukanda wa Ziwa mkoani humo.

“Watoto wanapaswa kwenda shule, ni haki yao, watoto wengi wapo mitaani wakifanya kazi wakiwa na umri mdogo, nawaagiza polisi mfanye msako mkali, nyumba kwa nyumba, kuwakamata wazazi ambao watoto wao wapo ziwani wakipara samaki, muwakamate,” alisema Lugola.

Waziri Lugola amemaliza ziara yake Mkoani Rukwa, ambapo alitembelea Wilaya na majimbo yote Mkoani humo, akisikiliza kero mbalimbali za wananchi pamoja na kutembelea miradi mbalimbali ya taasisi zilizopo ndani ya Wizara yake.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa