• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Waziri Mkuu Aanza Ziara Rukwa

imewekwa Tar: December 14th, 2022

MAJALIWA : HALMASHAURI TUMIENI FEDHA ZA NDANI KUKAMILISHA MIRADI

Na. OMM Rukwa

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameanza ziara ya kikazi katika Mkoa wa Rukwa ambapo ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule ya Sekondari ya Paramawe na hospitali ya Wilaya iliyopo Wilayani ya Nkasi.

Akiwa katika Shule ya Sekondari Paramawe leo (Desemba 14,2022) inayojengwa kupitia mradi wa SEQUIP ambapo ameweka jiwe la msingi la mradi huo uliogharimu Shilingi Milioni 470 kujenga vyumba nane vya madarasa,maabara,maktaba na matundu ya vyoo.

Akizungumza baada ya kukagua ujenzi huo, Waziri Mkuu amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo Rashid Mchatta kumsimamia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi William Mwakalambile ili ahakikishe anakamilisha maeneo ya ujenzi wa shule hiyo kwa kutumia mapato ya ndani.

“Milioni 470 zimetumika na mmetumia zingine za halmashauri lakini miundombinu bado. Nataka shule hii ikamilike na Januari 2023 wanafunzi waingie” Alisema Majaliwa

Kuhusu ujenzi wa hospitali ya Wilaya Nkasi, Waziri Mkuu aliewaeleza wananchi kuwa serikali itaendelea kukamilisha miradi yote ya afya ikiwemo kuhahikisha vifaa tiba vinapatikana kwa ajili ya wananchi kupata huduma.

Aidha, Waziri Mkuu amemwagiza Naibu Katibu Mkuu  Tamisemi -Afya kukutana na uongozi wa halmashauri ya Nkasi ili kujua kwanini mradi ya ujenzi wa majengo saba ya hospitali ya wilaya haujaanza wakati tayari fedha zilikwishatolewa na serikali.

“Naibu Katibu Mkuu Tamisemi urudi hapa Nkasi kesho kufuatilia kwanini majengo saba hayajaanza wakati fedha ipo” aliagiza Waziri Mkuu Majaliwa.

Katika hatua nyingine Majaliwa ameagiza Mkuu wa Mkoa huo na Katibu Tawala wa Mkoa kuitisha kikao cha mawakala wa mbolea mapema iwezekanavyo ili kuhakikisha wakulima wanapata pemebejeo hiyo muhimu kwa kuwa serikali imekwisha toa fedha za ruzuku .

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga alisema mkoa unaendelea na usimamizi wa shughuli za maendeleo na kuwa wananchi watapata huduma stahiki.

Waziri Mkuu kesho ataendelea na ziara yake kwenye wilaya za Kalambo na Sumbawanga.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa