• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

WAZIRI PINDI CHANA AZINDUA MIRADI YA MAENDELEO KALAMBO, RUKWA

imewekwa Tar: October 1st, 2024



Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Hazara Chana (Mb) amefanya uzinduzi wa miradi ya maendeleo yenye thamani ya jumla ya shilingi bilioni 1.8 katika Wilaya ya Kalambo Mkoa wa Rukwa leo Oktoba 1, 2024.

Akiwa katika siku ya kwanza ya ziara yake ya siku tatu Mkoani hapa, Mheshimiwa Chana amezindua mradi wa Maji wa Kilewani wenye thamani ya shilingi milioni 597.6. Mradi wa maji wa Kilewani ni miongoni mwa miradi ya maji iliyojengwa kwa fedha za Mfuko wa Taifa wa Maji (National Water Fund) na unahudumia wakazi wapatao 3, 847. Mradi huo umefikia asilimia 98 ya utekelezaji wake.

Miradi mingine iliyozinduliwa na Mheshimiwa Waziri Chana ni pamoja na mradi wa ujenzi wa Shule Mpya ya Sekondari Josephat Kandenge iliyoko Kata ya Mpombwe, mradi uliogharimu kiasi cha shilingi milioni 583.1 hadi kukamilika kwake.

Katika ziara hiyo Mheshimiwa Chana amezindua pia mradi wa ujenzi wa Shule mpya ya Msingi ya Namlangwa iliyoko Kata ya Lyowa wenye thamani ya shilingi milioni 638.


Akizungumza na wananchi wa Wilaya ya Kalambo, Mheshimiwa Waziri Chana amesema Serikali imedhamiria kutatua changamoto ya umbali wa upatikanaji wa huduma kwa kuhakikisha inasogeza huduma za maji, elimu na afya karibu zaidi na wananchi.

Mheshimiwa Pindi Chana amewataka wananchi kutunza miradi inayojengwa na Serikali ili azma ya huduma kusogezwa karibu na wananchi itimie. Ameeleza kuwa upatikanaji wa maji, elimu na afya karibu na makazi ya wananchi utaongeza ufanisi katika shughuli mbalimbali za ujasiriamali na kuongeza kipato cha wananchi.


Wananchi Wilayani Kalambo wameishukuru Serikali ya awamu ya sita kwa fedha za utekelezaji wa miradi hiyo.


Mheshimiwa Chana yuko ziarani Mkoani Rukwa, ziara itakayochukua siku 3.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa